Thursday 24 March 2011

RAIS KIKWETE ATEMBELEA WIZARA YA UCHUKUZI

 
Rais Jakaya Kikwete (katikati) akisalimiana kwa furaha na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usafirishaji wa Majini na Nchi Kavu( SUMATRA) Bw. Israel Sekirasa mara baada ya kuhitimisha ziara yake Wizara ya Uchukuzi leo jijini Dar es salaam. Wengine wanaoshuhudia ni Katibu mkuu wa Wizara ya Uchukuzi Eng. Omari Chambo (wa kwanza kushoto) akifuatiwa na Waziri wa Uchukuzi Omari Nundu.

Rais Jakaya Kikwete akizungumza na Watendaji wa Wizara, Idara, Mamlaka na Taasisi za Wizara ya Uchukuzi leo jijini Dar es salaam. Pamoja na mambo mengine amewataka viongozi hao kuzifanyia kazi changamoto zinazoikabili wizara hiyo zikiwemo uboreshaji wa huduma za reli, usafiri mijini,uboreshaji wa huduma za bandari, matengenezo ya viwanja vya ndege nchini na migogoro ya wafanyakazi.

No comments:

GEITA DOCUMENTARY

Contributors