Friday 19 October 2012

WALEMAVU WENGI HAWAJUI KUSOMA, KUANDIKA



ZAIDI ya asilimia 90 walemavu wa viungo wilayani Karagwe hawajui kusoma na kuandika kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo kunyanyapaliwa katika jamii.
Hayo yalibainishwa jana mjini hapa na Mwenyekiti wa Chama cha Walemavu (CHAWATA) wilayani hapa, Hashimu Muhamud, alipozungumza na waandishi.

Tuesday 16 October 2012

KAMANDA BARLOW KUAGWA LEO DAR ES SALAAM



BAADA ya kuagwa na maelfu ya watu katika Uwanja wa Nyamagana jijini Mwanza jana, leo aliyekuwa Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Mwanza, marehemu Liberatus Barlow ataagwa Dar es Salaam

Jana saa 4.15 asubuhi msafara wa magari kutoka Pasiansi, nyumbani kwa marehemu uliingia katika uwanja huo uliokuwa tayari umefurika watu kuanzia saa 2 asubuhi huku wengine wakiendelea kuingia.


Kuagwa kwa Barlow kulitanguliwa na Misa iliyoongoza na Padri Raymond Mayanga na baadaye watu mbalimbali walipata nafasi ya kutoa salamu zao. Na baada ya shughuli hiyo mwili huo ulisafirishwa kwenda Dar es Salaam iliko familia yake.

Ratiba Dar Leo mwili wa Kamanda Barlow unatarajiwa kuagwa kuanzia saa tano asubuhi katika Kanisa Katoliki Ukonga. Kwa mujibu wa taarifa ya Polisi, baada ya kuagwa, mwili utasafirishwa kwenda nyumbani kwao Kilema, Moshi Vijijini, Kilimanjaro kwa maziko yatakayofanyika kesho mchana kwa kufuata taratibu za kidini na kuhitimishwa na taratibu za kijeshi.

GEITA DOCUMENTARY

Contributors