Friday 6 June 2014

BUNGENI DODOMA: PICHA ZA MH. VICKY KAMATA AKIWA NDANI YA UKUMBI WA BUNGE.. SIKU CHACHE BAADA YA KUTOKA HOSPITALI.

Na Steven Mruma [Dodoma]

        Mh. Vicky Kamata aliwasili Bungeni Dodoma na kama ilivyo ada alipokewa vizuri na kila mbunge aliyekutana nae. Wabunge wengi walimpa pole baada ya kuugua siku chache kabla ya ndoa yake na kumtakia kila la kheri, huku wengi wakiamini kilichotokea ni mpango wa Mungu na kua Ndoa yake ipo na itakuwepo siku yoyote Mungu akiamua kulitimiza kusudi lake juu ya Mh. Vicky Kamata..       Wakati wabunge wengi wakimuhurumia na kudhani kua kutofungwa kwa ndoa yake kungemgharimu siku nyingi kurudi katika hali ya kawaida, ilikua ni tofauti kabisa kwa upande wa Mh. Vicky Kamata kwani muda wote alikua na amani na kwamba hakujiskia vibaya kama wengi walivyodhani na ndio maana ilichukua muda mfupi sana na aliweza fika Bungeni na kazi ya kuwatumikia wananchi wake wa Geita na Tanzania kwa ujumla ilianza mara moja na kwamba bado anaamini kilichotokea ni mpango wa Mungu na kwamba Mungu hakosei na anamini Muda si mrefu atafunga ndoa na kila mtu atashuhudia na mkono wa Mungu utasiamama juu ya ndoa yake.
Mh. H. Kigwangala akiwa amemkumbatia Mh. Vicky Kamata baada ya kuingia ukumbi wa Bunge mjini Dododma

Mh. Vicky Kamata akiteta jambo na baadhi ya wabunge wenzake ndani ya ukumbi wa Bunge mjini Dodoma
Mh Vicky Kamata akiwa amekumbatiwa na mbunge mwenzake
   

GEITA DOCUMENTARY

Contributors