Friday 2 April 2021

MAKALA MAALUM KWA WAFUGAJI WA KUKU: ZIFAHAMU TARATIBU NA RATIBA ZA UCHANJAJI WA KUKU KUANZIA VIFARANGA NA KUKU WAKUBWA.


Mtaalam wa Mifugo akiwapa chanjo vifaranga.
TARATIBU NA RATIBA ZA UCHANJAJI
    Wakati wa kutayarisha mpango wa kuchanja kuku kwa ajili ya kinga dhidi ya magonjwa, kuna vipengele vikuu sita Ambavyo unatakiwa uvifahamu na kuvizingatia. Vipengele hivyo ni kama ifuatavyo:
Kuku wakienyeji ni rahisi sana kuwafuga tofauti na wakisasa.
1. Vifaranga vinavyoanguliwa kwa pamoja:
 Iwapo una kundi zaidi ya moja la vifaranga wanaoanguliwa,
Weka utaratibu wa chanjo ambao utapunguza uwezekano wa magonjwa kuenea shambani. Hivyo basi,
Zipo namna nyingi za uchanjaji wa kuku zingine zinahitaji utaalam
Hakikisha vifaranga na kuku wote wanapata chanjo kwa pamoja.
2. Umri wa kuchanja kuku:
Kwa kuku ambao wanatarajiwa kutaga mayai au kuwa kuku wazazi, chanjo
nyingi hutolewa si zaidi ya mwezi mmoja kabla ya kuku kuanza kutaga. Pia kuna baadhi ya chanjo ambazo haziruhusiwi kwa kuku wadogo. (Angalia Ratiba).
3. Magonjwa muhimu katika eneo husika:
Ni muhimu sana kuelewa magonjwa ya kuku yaliyopo katika eneo lako kabla ya kuandaa programu ya uchanjaji, hasa kwa yale magonjwa ambayo chanjo zenye
Vimelea hai hutumika. Hivyo basi, sio busara kuanza kutumia chanjo za aina hii katika maeneo ambayo
Ugonjwa huo haujawahi kuripotiwa.
4. Hali ya kiafya ya kuku watakaochanjwa:
 Usiwape chanjo kuku ambao wanaonyesha dalili za kuathirika kwa mfumo wa hewa au wanaonyesha kuwa na minyoo au wadudu wengine. Kwa kuku walio na dalili hizi chanjo zinaweza kuleta madhara na zisifanye kazi.
5. Aina ya kuku watakaochanjwa:
Kuku wanaofugwa kwa ajili ya nyama wanahitaji kinga ya muda mfupi, hivyo basi chanjo moja inaweza kutosha kabla ya kufikia umri wa kuuzwa. Lakini kuku wa mayai na kuku wazazi wanahitaji programu ya chanjo ambayo itawakinga na magonjwa kwa kipindi chote wanapokua na kutaga. (Zingatia Ratiba).
6. Historia ya Magonjwa katika shamba:
Kabla ya kuandaa mpango wa chanjo, lazima ufahamu ni
Magonjwa gani yaliyoenea katika shamba.
a) Kama unataka kuingiza kuku wapya kutoka mahali ambako ugonjwa umeshawahi kutokea,
kuku hao wachanjwe wiki 3 kabla ya kuwaingiza shambani
b) Iwapo utatumia chanjo yenye vimelea hai, hakikisha kwamba magonjwa hayo yameshawahi
kutokea katika shamba husika. Usitumie chanjo hizi katika shamba ambalo ugonjwa huo
haujawahi kutokea au kutambuliwa.
c) Wasiliana na mashamba jirani kufahamu iwapo wanatumia chanjo zenye vimelea hai. Toa taarifa
kwa mamlaka za mifugo iwapo unapanga kutumia chanjo hizo katika eneo lako. Pata ushauri wa daktari.

TARATIBU ZA UCHANJAJI
Mambo muhimu ya kuzingatia:                                                                                         
  •Hakikisha unazingatia kwa makini masharti ya mtengenezaji wa chanjo: jinsi ya kuhifadhi, kutayarisha na njia inayotumika kumchanja kuku. Wakati wote zingatia masharti ya mtengenezaji kuhusu uhifadhi wa chanjo ili isipoteze nguvu.                                                     
                     

GEITA DOCUMENTARY

Contributors