Monday 16 December 2013

Sunday 15 December 2013

Mazishi ya Nelson Mandela yanaendelea katika kijiji cha Qunu katika mkoa wa Eastern Cape.

Na Steven Mruma kwa msaada wa BBC Swahili.

    Mazishi ya Nelson Mandela yanaendelea katika kijiji cha Qunu katika mkoa wa Eastern Cape na kumaliza wiki moja ya maombolezi ya shujaa wa Afrika mwendazake Nelson Mandela.

      Takriban watu 4,500 ikiwemo wageni wa kimataifa wanahudhuria mazishi hayo ambayo ni ya mchanganyiko wa tamaduni za kale na mambo ya kisasa.
Familia ya Mandela ilikesha wakijiandaa kwa mazishi ya leo huku kukiwa na muimbaji ambaye atakuwa anaita mizimu ya mababu wa kale na pia wakiongelesha mwili wa Mandela kumwambia kuwa sasa anazikwa. Ni kuambatana na tamaduni na mila za watu wa ukoo wa Mandela wa Thembu.
     Viongozi wa Afrika, familia na marafiki wametoa heshima zao za mwisho kwa hayati Nelson Mandela katika mazishi yake ya kitaifa katika kijiji cha Qunu katika mkoa wa Cape Mashariki. Mandela alikuwa rais wa kwanza mzalendo wa Afrika Kusini.
Rais Jacob Zuma amesema kuwa wakati safari ndefu ya Mandela kuelekea uhuru imekwisha, raia wa Afrika Kusini wana jukumu la kuendeleza sera zake na urithi wake.
Jeneza lenye mwili wa mzee Nelson Mandela Likiwa limefunikwa na ngozi ikiwa ni ishara ya heshima ya kabila la Thembu

Jeshi likisindikiza msafara wenye mwili wa Mzee Mandela


PICHA ZA SEHEMU ATAKAYOZIKWA MZEE MANDELA LEO.

Na Steven Mruma.

   WAKATI TAARIFA KAMILI YA MAZISHI YA MZEE MANDELA IKIANDALIWA KUPITIA NJIA MBALIMBALI, TUMIA MUDA KUANGALIA PICHA ZA SEHEMU ATAKAYOZIKWA MZEE MANDELA KIJIJINI KWAO QUNU.





GEITA DOCUMENTARY

Contributors