Sunday 10 May 2015

PICHA ZA MAHAFALI YA JULIANA MMOJA WA WAIMBAJI WA KUNDI LA J.SISTERS ALIPOHITIMU SHAHADA YA KWANZA YA PHAMARCY HUKO NCHINI MAREKANI.

Steven Mruma,,

      Mmoja kati ya waimbaji wa kundi la muziki wa injili la J.Sisters, Juliana Julius Mshama amehitimu mafunzo ya shahada ya kwanza ya Pharmacy katika chuo cha Liberty universirty of lynchburg va. Amerika huko nchini marekani. Pamoja na Juliana chuoni hapo pia wamesoma ndugu zake wawili Jennifer na Jackline huku mdogo wao Jesca akitarajia kujiungana na chuo hicho hivi karibuni.
      Juliana na ndugu zake wamekua miongoni mwa wasanii wa muziki wa injili wachache wasomi zaidi wakiwakilisha vema kundi lao la muziki J.Sisters waliotamba na nyimbo nyingi ikiwemo shuka bwana.

ZIFUATAZO NI BAADHI YA PICHA KATIKA MAHAFALI ILIYOFANYIKA HUKO NCHINI MAREKANI
Juliana J. Mshama mmoja wa waimbaji mahiri wa kundi la J.Sisters

Juliana (aliyevaa joho) akiwa na ndugu zake Jennifer na Jackline pamoja na  jamaa na marafiki zake wakati wamahafali yake pamoja na Baba yao Julius Mshama (mwenye kofia nyeusi)







GEITA DOCUMENTARY

Contributors