Friday 28 December 2012

UJIO WA TEKNOLOJIA YA DIJITALI UTAWAKOMBOA WASANII?


KUMEKUWA na hofu miongoni mwa wasanii na Watanzania wengine kuhusu ujio wa mpango wa dijitali kwamba ni nani atasalimika.
Wasanii ninyi mtakuwa wa kwanza kusalimika kwani hivi sasa mtaweza kuuza kazi zenu bila masharti kuwa lazima sura za fulani na fulani ziwepo.
Bila shaka mfumo huu wa dijitali sasa utakuwa mkombozi na mwarobaini kwa wacheza filamu nchini.
Ni kweli utakuwa mkombozi kwa sababu kuu moja tu, kwani hivi sasa msanii/ kikundi cha wasanii kinaweza kujikusanya na kuamua kucheza filamu ya hadithi watakayotunga na kukubaliana bila kujali ndani ya filamu hiyo msanii gani mwenye jina kubwa amecheza na wataweza kuiuza katika luninga na kujipatia mkate wao wa kila siku.
Kwakuwa Tanzania inatarajiwa kuingia katika idadi ya nchi ambazo zitakuwa zimetekeleza kwa vitendo maazimio ya Tume ya Kimataifa ya Mawasiliano ( ITU), kwa kuchukua uamuzi wa kutoka katika mfumo wa utangazaji wa analojia na kuingia katika mfumo wa dijitali, ukoloni wa filamu kuuzika ama kuchezwa na wasanii /msanii nyota sasa utakufa kwa kufuatia mfumo huu wa dijitali.

GEITA DOCUMENTARY

Contributors