Friday 13 December 2013

TAZAMA PICHA YA HALI HALISI INAYOENDELEA NCHINI AFRIKA KUSINI KWENYE MSIBA WA MZEE NELSON MANDELA.

Rais wa Afrika Kusini Jacob Zuma akitoa heshima za mwisho

Rais Jacob Zuma akiondoka eneo la Union Building jijini pretoria, kwa nyuma ni Graca Machel alivaa nguo nyeusi
Rais wa Zimbabwe Robart Mugabe naye alikuwepo kutoa heshima za mwisho kwa aliyekuwa Rais wa Afrika Kusini Nelson Mandela
Rais wa Sli Lanka Mahinda Rajapaska akiondoka baada ya kutoa heshima za mwisho
Aliyewahi kuwa Rais wa Afrika Kusini Thabo Mbeki akitoa heshima za mwisho
Mjane wa Mzee Nelson Mandela Graca Machel akiuaga mwili wa aliyekuwa mume wake mzee Nelson Mandela
Aliyewahi kuwa mke wa Nelson Mandela Winnie Mandela akilia kwa huzuni baada ya kuuaga mwili wa Mzee Nelson Mandela
Mwanamitindo mashuhuri Duniani Naomi Campbell akiwa na simanzi baada ya kuuga mwili wa marehemu mzee Nelson Mandela
Winnie Mandela akitoka eneo la kuuaga mwili wa Mzee Mandela , Winnie pia aliwahi kuwa mke wa Mzee Mandela
Maofisa wa jeshi wakijiandaa kubeba jeneza lililobeba mwili wa Mzee Mandela
Maofisa wa Jeshi wakiwa wamebeba jeneza lenye mwili wa Mzee Mandela

Monday 9 December 2013

TAZAMA PICHA ZA MAADHIMISHO YA MIAKA 52 YA UHURU WA TANGANYIKA [SASA TANZANIA] UWANJA WA UHURU


Rais Kikwete akiwasili uwanja wa uhuru

Wimbo wa Taifa ukiimbwa

Rais akikagua gwaride

ukaguzi wa gwaride ukiendelea
Rais wa Zanzibar na M/kiti wa baraza la mapinduzi Ali M. Shein akisalimiana na Makamu wa Rais wa Jamuhuri wa muungano wa Tanzania Gharib Bilal

Rais Kikwete akihutubia wananchi
Vikosi vya usalama vikiwa tayari kwa ukaguzi

Gwaride la kikosi cha akina Wanawake kikitoa heshima zake kwa gwaride la mwendo wa haraka


Kikosi cha FFU wanaume wakipita kwa mwendo wa kasi katika gwaride la heshima wakati wa maadhimisho ya miaka 52 ua uhuru wa Tanganyika.

RAIS KIKWETE AONGOZA MAADHIMISHO YA MIAKA 52 YA UHURU WA TANGANYIKA UWANJA WA UHURU.

Bendera zikipepea nusu mlingoti ikiwa ni ishara ya kuomboleza kifo cha Mzee Nelson Mandela.
Rais Kikwete akiwasili uwanja wa uhuru katika maadhimisho ya miaka 52 ya uhuru wa Tanganyika

Vikosi vya usalama katika gwaride la heshima kuadhimisha miaka 52 ya uhuru wa Tanganyika.

Vijana wa vikosi vya usalama wakiwa kazini katka Gwaride la heshima la kuadhimisha miaka 52 ya uhuru wa Tanganyika
Vikosi vya usalama katika gwaride la heshima.

Watoto wa halaiki wakitoa burudani ya aina yake katika maadhimisho ya miaka 52 ya uhuru katika uwanja wa uhuru leo.
Dar es Salaam.
     Happy birthday Tanganyika’. Miaka 52 imetimia tangu Tanganyika (sasa Tanzania), kupata uhuru wake kutoka kwa wakoloni wa Kiingereza, Desemba 9, mwaka 1961.
Kama ilivyo ada, katika maadhimisho hayo yatakayofanyika kwenye Uwanja wa Taifa Dar es Salaam, Rais Jakaya Kikwete anatarajia kukagua gwaride la vikosi mbalimbali vya ulinzi na usalama ambavyo pia vitatoa heshima kwa kiongozi huyo kwa mwendo wa pole na haraka. Baadaye kikosi cha anga kitatoa heshima zake na kufuatiwa na burudani mbalimbali ikiwamo ngoma na michezo ya halaiki. Sherehe hizo pia zitahudhuriwa na wageni mbalimbali waalikwa wa ndani na nje ya nchi, wakiwamo mabalozi wanaoziwakilisha nchi zao hapa nchini.
Katika sherehe hizo, Rais Kikwete hutoa msamaha kwa wafungwa na mwaka jana aliwasamehe wafungwa 3,814 waliokuwa na umri zaidi ya miaka 70, wenye ulemavu wa mwili na akili, magonjwa kama Ukimwi, kifua kikuu na saratani ambao wako kwenye hatua ya mwisho ya ugonjwa,
Wengine ni wafungwa wa kike walioingia na mimba gerezani na walioingia na watoto wanaonyonya na wanaotumikia kifungo kisichozidi miaka mitano ambao hadi siku ya msamaha, walikuwa wametumikia robo ya vifungo vyao.
Katika maadhimisho hayo mwaka jana, yaliyohudhuriwa na viongozi 14 wa kutoka Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika (SADC), Rais Kikwete aliwataka Watanzania kujivunia na kuyaenzi mafanikio ya kisiasa, kiuchumi na kijamii yaliyopatika tangu nchi ilipopata uhuru.

GEITA DOCUMENTARY

Contributors