Saturday 20 December 2014

PICHA ZA MAHAFALI YA CHUO CHA WAANDISHI WA HABARI DSJ. AMBAPO MGENI RASMI ALIKUA MH. VICKY KAMATA.

Na Steven Mruma [Dar es salaam] 

      Jana yalifanyika mahafali ya 20 ya chuo cha waandishi wa habari cha DSJ na mgeni rasmi alikua ni Mh. Vicky Kamata.Wakati akihutubia Mh. Vicky aliwaasa waandishi hao waliohitimu  wazitumie kalamu zao vizuri kuijeNga na kuilinda amani ya nchi ambayo kwa kiasi kikubwa inaweza kuvurugika iwapo hawatatumia vizuri kalamu zao kwa maslahi mapana ya taifa.
    Katika mahafali hiyo iliyofana na ya aina yake pia iliisha kwa Mgeni Rasmi kuimba wimbo wake uliomtambulisha katka tasnia ya muziki wa wanawake na maendeleo.
    Ikumbukwe kua Mh. Vicky Kamata ni pamoja kua ni mbunge wa viti maalum mkoa wa Geita lakini ni mwanamuziki aliyewahi kutamba na wimbo wa wanawake na maendeleo, Mapenzi na Shule, Fitina, Nimeolewa..nk.  na sasa ameingiza sokoni albamu yake mpya inayotwa MOYO WA MTU KICHAKA.

ZIFUATAZO NI BAADHI YA PICHA ZA MAHAFALI HAYO YA DSJ

SAFARI ILIANZIA NJE YA OFISI ZA VICTORIA FOUNDATION KUELEKEA CHUO CHA DSJ

MGENI RASMI MH. VICKY KAMATA AKIWASILI CHUO CHA DSJ

HAPA AKIMSIKILIZA MKUU WA CHUO J. RUPEPO HAYUPO PICHANI NA KULIA NI MRATIBU WA MAFUNZO DADA JOYCE MBOGO

MGENI RASMI AKISAINI KITABU CHA WAGENI

AKISAIDIWA KUVISHWA JOHO MAALUM NA MRATIBU WA MAFUNZO JOYCE MBOGO


MGENI RASMI AKITOKA CHUONI KUELEKEA UKUMBI ULIOANDALIWA KWA AJILI YA MAHAFALI

BAADA YA KUWAASILI NJE YA UKUMBI ULIOFANYIKA MAHAFALI KUTOKA KUSTOTO NI MKUU WA CHUO NDUGU JOACHIM RUPEPO, MRATIBU WA MAFUNZO DADA JOYCE MBOGO NA MGENI RASMI MH. VICKY KAMATA

KUELEKEA UKUMBINI

BAADA YA KUWASILI WALIPOKEWA KWA NDELEMO NA VIFIJO NA WAGENI PAMOJA NA WAHITIMU NA WANACHUO WANAOBAKI.

WIMBO WA TAIFA UKIIMBWA

RISALA YA WAHITIMU

SEHEMU YA WAHITIMU WALIOHITIMU MAFUNZO YA UANDISHI WA HABARI

MKUU WA CHUO NDUGU JOACHIM RUPEPO AKISOMA MUHTASARI NA HISTORIA FUPI YA CHUO CHA DSJ

MGENI RASMI MH. VICKY KAMATA AKIHUTUBIA WAHITIMU WAGENI WAALIKWA PAMOJA NA WANACHUO WANAOBAKI.

HOTUBA IKIENDELEA


SEHEMU YA WAHITIMU

WAHITIMU

WAHITIMU WAKIWA TAYARI KUTUNUKIWA VYETI KATIKA NGAZI MBALIMBALI NA KOZI MBALIMBALI

WAHITIMU WAKIWAPA MIKONO MEZA KUU

WAHITIMU WALIOFANYA VIZURI KATIKA KOZI MBALIMBALI WAKIPEWA VYETI MAALUM VYA HESHIMA

UTOAJI WA VYETI MAALUM UKIENDELEA



MIONGONI MWA WALITUNUKIWA VYETI VYA HESHIMA NI MWANAHARAKATI KIJANA JAMES MWAKIBINGA


MGENI RASMI MH. VICKY KAMATA AKISHUKURU BAADA YA KUPATIWA CHETI MAALUM CHA HESHIMA NA SHUKRANI.

PICHA YA PAMOJA MEZA KUU NA WAHITIMU




PICHA YA PAMOJA MEZA KUU NA WAKUFUNZI NA WAFANYAKAZI WA CHUO CHA DSJ

BAADA YA KUMALIZA PICHA ZA PAMOJA HAPA MGENI RASMI MH. VICKY KAMATA AKIAGANA NA UONGOZI WA CHUO

NA HAPA MGENI RASMI MH. VICKY KAMATA ALIKUA AKIIMBA LIVE WIMBO WA WANAWAKE NA MAENDELEO. IKUMBUKWE KUA MH. VICKY PAMOJA KUA NI MBUNGE WA VITI MAALUM MKOA WA GEITA ILA NI MUIMBAJI MAHIRI.

PICHA ZA PAMOJA NA MASHABIKI WAKE KABLA YA KUONDOKA ENEO LA MAHAFALI



Tuesday 16 December 2014

PICHA: PIGO CHADEMA: WANACHAMA ZAIDI YA 35 BAWACHA WAHAMIA CCM GEITA BAADA YA KUCHOSHWA NA UBABAISHAJI WA CHAMA HICHO.

 Na Steven Mruma
       Hivi karibuni wakati wa kampeni za uchaguzi kikundi cha akina mama zaidi ya 35 wa BAWACHA kutoka chama cha Chadema, waliamua kukikimbia chama hicho na kukimbilia kwa Baba na Mama aliyewalea CHAMA CHA MAPINDUZI baada ya kuchochwa na sera chafu na ubabaishaji wa chama hicho cha Chadema.
      Mara baada ya kukutana na Mh. Vicky Kamata wakati akiendelea na kampeni za kuwanadi wagombea wa serikali za mitaa Geita walimueleza kuwa sasa wanajiskia amani kurudi nyumbani baada ya kukichoka chama hicho walichokikimbia cha Chadema. 

Baadhi wa waliokuwa wakina mama kutoka chama cha chadema Bawacha waliohamia CCM wakimueleza jinsi walivyoishi katka shida nyingi wakati wakikitumikia chama cha chadema

Baada ya kurudisha kadi za Chadema Mh. Vicky Kamata aliwakabidhi kadi za CHAMA CHA MAPINDUZI

Mh. Vicky akiwa na wanachama wa CHAMA CHA MAPINDUIZI mara baada ya kuwakabidhi kadi za CCM wakinamama waliokihama chama cha chadema na kuhamia CCM

Baadhi wa waliokuwa wakina mama kutoka chama cha chadema Bawacha waliohamia CCM baada ya kukabidhiwa kadi za CCM na Mh. Vicky Kamata.

GEITA DOCUMENTARY

Contributors