Friday 2 November 2012

MAFUTA BADO UTATA



WAKATI Kampuni ya uratibu ya uagizaji wa mafuta kwa pamoja (PIC) ikipigiana chenga na Mamlaka ya Udhibiti wa Nishati na Maji (Ewura) kuhusu uhaba wa mafuta nchini, serikali imeagiza kusitisha kusafirisha mafuta nje ya nchi.
Agizo hilo la serikali lilitolewa jana na Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Eliackim Maswi, alipokutana na Bodi ya PIC pamoja na Ewura mbele ya waandishi wa habari na kuwataka waeleze sababu za kuadimika kwa nishati hiyo nchini.

TOA MAONI YAKO YA KATIBA MPYA KWA SMS SASA..



TUME ya Mabadiliko ya Katiba imetangaza namba nne za simu za mkononi ambazo wananchi kwa sasa wanaweza kuzitumia kutuma ujumbe mfupi wa maandishi ‘sms’ kutoa maoni yao kuhusu Katiba mpya.
Kwa mujibu wa taarifa ya tume hiyo kwa vyombo vya habari iliyotolewa jana, namba ambazo wananchi wanaweza kutuma maoni yao ni 0715-081508, 0767-081508, 0787-081508 na 0774-081508.

Monday 29 October 2012

VINARA WA ROCK CITY MARATHON



MWANARIADHA anayekuja juu kwa kasi, Mwita Kopiro, wa Mwanza na Mary Naali wa Arusha, jana waliibuka washindi katika mbio za Nusu Marathon za Rock City zilizofanyika jijini Mwanza jana.

Mwita alishinda mbio hizo kwa upande wa wanaume, akitumia saa 1:04:02, huku Mary anayetoka klabu Skytel akishinda kwa wanawake akitumia saa 1:16:33.

Waliofuatia kwa wanawake ni Sarah Ramadhan Arusha (1:16:37), Anastasia Msindai Arusha (1:19:05), Failuna Mohamed Arusha (1:19:20), Musengimana kutoka Rwanda (1:22:09), Banuelia Brighton Holili Kilimanjaro (1:22:15), Dorcas Jepchirchir Kenya (1:26:12), Sarah Kavina JKT Arusha (1:36:37), Furaha Sambeki Tanzania (1:36:55), na Grece Jackson (1:40:53).

GEITA DOCUMENTARY

Contributors