Friday 21 December 2012

SERIKALI IGUSWE NA HALI YA SAJUKI



MSANII maarufu wa filamu nchini, Sadick Kilowoko ‘Sajuki’, kwa muda mrefu amekuwa akisumbuliwa na matatizo ya kiafya hadi kupelekwa nchini India kwa matibabu.
Baada ya matibabu ya muda mrefu, msanii huyo alirejea nchini akiwa amepata nafuu kubwa tofauti na wakati anakwenda hivyo akawashukuru wote waliofanikisha gharama za safari yake.
Lakini pamoja na kurejea nchini akiwa amepata nafuu kubwa, bado akatakiwa kurejea India kwa uchunguzi na matibabu zaidi, kitu ambacho pia kinahitaji gharama kubwa ya fedha.
Kwa mujibu wa rafiki yake wa karibu (Dennis Sweya), Sajuki anahitaji kiasi cha shilingi mil. 28, ikiwa ni gharama za kwenda na matibabu nchini India.
Zimebaki shilingi mil. 21 kupata kiasi cha fedha kinachohitajika kwa ajili ya msanii huyo kwenda India kwa matibabu zaidi katika kupigania uhai wake.

Wednesday 19 December 2012

ANASWA NA NDUMBA MAHAKAMANI


Mganga wa kienyeji aliyefahamika kwa jina la RAJAB ZUBERI (30), mkazi wa Kerege, Muheza, Tanga, akiwa chini ya ulinzi wa Wanausalama  katika Mahakama ya Hakimu Mkazi, Kisutu jijini Dar es Salaam, baada kifaa cha upekuzi kumnasa mganga huyo akiwa na vifaa vyake vya uganga ambavyo alikuwa amekuja navyo mahakamani hapo kwa ajili ya kufanyia mambo ya kishirikina katika kesi moja inayomkabili  mmoja wa washtakiwa mahakamani hapo. 

KUKAMATWA KWA MWIZI MKUU WA MAGARI NA VIFAA VYA MAGARI

 Rama Jangiri ambaye ndiye kiongozi wa genge la waiba vifaa vya magari jijini Dar.


Hili ndiyo tukio halisi la kukamatwa kwa Rama Jangiri akiwa kwenye hotel ya Farway baada ya kufuatiliwa kupitia mtandao kufuatia tukio la wizi wa vifaa vya gari na pia Compyuta na simu kutoka kwenye gari la mmoja wa wakazi wa jiji la Dar ambalo sasa wamiliki wa magari wamekuwa na wasiwasi mkubwa kila wanapokuwa wamepaki magari yao kufuatia kushamirikwa wizi wa vifaa mbalimbali uliokuwa ukifadhiliwa na bwana Rama na kundi lake.
Rama Jangiri akifikishwa kwenye kituo cha Polisi Mbezi Juu mara baada ya kukamatwa.
 
 
 
 
Picha na teentz 

 


Sunday 16 December 2012

MUNGU AILAZE ROHO YA MAREHEMU AMINA SINGO MAHALA PEMA PEPONI

Aliyekuwa mtangazaji wa kituo cha utangazaji cha TIMES FM  Amina Singo afariki dunia. Amina alikuwa akitangaza kipindi cha Afro Vibes kinachorushwa na kituo hicho.
 
 
                    "Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema peponi,Amen"

GEITA DOCUMENTARY

Contributors