Saturday 23 April 2011

MIAKA 47 YA MUUNGANO WETU


Siku ya Jumatatu tarehe 26/04/2011, Tanzania itaadhimisha miaka 47 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar ulioasisiwa tarehe 26/04/1964 kwa yaliyokuwa Mataifa mawili, Jamhuri ya Tanganyika na Jamhuri ya Watu wa Zanzibar kuungana na kuzaliwa Taifa moja la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Vikosi vya Ulinzi na Usalama, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete atakuwa mgeni rasmi katika kilele cha Maadhimisho ya sherehe hizo Mwaka huu ambazo kitaifa zitafanyika kwenye Uwanja wa Amaan Mjini Zanzibar.

Mbali na Rais Kikwete, Viongozi mbalimbali wa Kitaifa,Mabalozi wanaowakilisha nchi zao hapa nchini pamoja na wananchi kutoka Mikoa mbalimbali wanatarajiwa kushiriki katika Maadhimisho hayo.

Mkataba wa Muungano ulitiwa saini na aliyekuwa Rais wa Tanganyika, Marehemu Mwalimu Julius KambarageNyerere na aliyekuwa Rais wa Zanzibar, Marehemu Sheikh Abeid Amani Karume tarehe 22 Aprili 1964 Zanzibar.

Siku ya Jumatatu tarehe 26 Aprili, 1964, viongozi wa nchi zote mbili walikutana katika ukumbi wa Karimjee Jijini Dar es Salaam na kubadilishana Hati za Muungano.

Thursday 21 April 2011

Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akipiga ngoma muda mfupi baada ya kuwasili katika hoteli ya Kilimanjaro Kempinski kuhudhuria kikao cha Wakuu wa nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki kilichomalizika jijini Dar es Salaam.Pembeni ya Rais ni wasanii wa kikundi cha ngoma kutoka Burundi(picha na Freddy Maro).

Tuesday 19 April 2011

ATHARI ZA MVUA DAR

Mafuriko nje ya jengo la Mayfair Plaza

WAKUU WA NCHI ZA JUMUIYA YA AFRIKA MASHARIKI WAKUTANA DAR

 Rais Jakaya Kikwete akiongea na Omary Nundu Waziri wa Uchukuzi kutoka Tanzania wa pili kutoka kulia, mara baada ya kuwasili katika katika hoteli ya Kempiski jijini Dar es salaam tayari kwa kupokea wageni wake, ambapo mkutano wa wakuu wa nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki unafanyika kuanzia leo, wakuu hao watajadili mambo mbalimbali ya kimaendelea kuhusu Jumuiya ya Afrika Mashariki ikiwa ni pamoja na kuchagua Katibu Mkuu mpya, atakayechukua nafasi ya Juma Mwapachu aliyekuwa Katibu Mkuu wa Jumuiya hiyo kutoka Tanzania, Katika picha katikati ni Balozi Chirau Ali Makwere Waziri wa biashara wa Jamhuri ya Kenya na kulia ni Dr. Shukuru Kawambwa Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi wa Tanzania.

 Maofisa mbalimbali wakisubiri kuanza kwa mkutano kutoka kulia ni Asther Mkwizu Mwenyekiti wa Mfuko wa sekta binafsi Tanzania, Mh. Abdallah Mwinyi Mbunge wa Afrika Mashariki kutoka Tanzania na mwisho ni Robert Bayigamba Mwenyekiti wa sekta binafsi nchini Rwanda.

Mawaziri wa Tanzania na Kenya wakijadili jambo kabla ya kuanza kwa kikao cha wakuu wa nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki katika hoteli ya Kilimanjaro Kempinski leo asubuhi kutoka kulia ni Dr. Harrison Mwakyembe Naibu waziri wa Ujenzi, Dr Shukuru Kawambwa Waziri wa Elimu na mafunzo ya ufundi, Omary Nundu Waziri wa Uchukuzi na Balozi Chirau Ali Makwere Waziri wa Biashara wa Jamhuri ya Kenya

MUSEVENI AWASILI DAR


Rais wa Uganda Yoweri Museveni akiwasili Mlimani City kwenye mkutano wa uwekezaji Afrika. Kulia ni Waziri wa Maji Prf. Mark Mwandosya na Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki Balozi Juma Mwapachu.

JOSEPH MGASA AMTEMBELEA MHE.KAMATA NYUMBANI KWAKE

 Mhe. Vicky Kamata akiwa na bibi yake, Bi.Celina katika pozi

 Joseph Mgasa ambaye ni lecture wa chuo cha Glasgow nchini Uingereza alipomtembelea Mhe.Vicky Kamata nyumbani kwake kijitonyama jijini Dar es Salaam.

 Mhe.Vicky Kamata, Joseph Mgasa na Revo katika picha ya pamoja

 Revo and Uncle Joe

MAKAMU WA RAIS ATIA SAINI KITABU CHA MAOMBOLEZO YA ALIYEKUWA MAKAMU WA RAIS WA BRAZIL

 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohamed Gharib Bilal, akisaini katika kitabu cha rambirambi wakati alipofika kwenye Ofisi za Ubalozi wa Brazil nchini, kuweka saini katika kitabu hicho maalum kutokana na kifo cha Makamu wa Rais wa zamani wa nchi hiyo,Jose Alencar da Silva, aliyefariki dunia hivi karibuni. 

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohamed Gharib Bilal (kushoto) akizungumza na Balozi wa Brazil nchini, Francisco Soares Carlos Luz, wakati Makamu alipofika kwenye Ofisi za ubalozi huo Dar es Salaam, kwa ajili ya kutia saini katika kitabu cha rambirambi cha aliyekuwa Makamu wa rais wa zamani wa Brazil, Jose Alencar da Silva, aliyefariki hivi karibuni nchini humo. Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais


Monday 18 April 2011

WAZIRI MKUU AKUTANA NA WAWEKEZAJI NA KUKAGUA MASHAMBA YA NYUKI NA KARANGA DODOMA

 Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akizungumza na wakwekezaji kutoka China, ofisini kwake, mjini Dodoma 

Waziri Mkuu Mizengo Pinda na mkewe Tunu (kulia) wakikagua shamba la karanga na mahindi, eneo la Zuzu,Dodoma.

Waziri Mkuu Mizengo Pinda na mkewe Tunu wakikagua mizinga ya nyuki kwenye shamba eneo la Zuzu, Dodoma. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

GEITA DOCUMENTARY

Contributors