Wednesday 8 August 2012

Vifo vya wajawazito, watoto vyakithiri Kigoma


MKOA wa Kigoma unakabaliwa na changamoto ya vifo vya wajawazito na watoto wa chini ya miaka mitano kwa sababu wajawazito wengi hujifungulia majumbani.
Mganga Mkuu wa Hospitali ya Mkoa wa Kigoma (Maweni) Dk. Leonard Sumbi alisema hayo wakati wa mkutano wa wadau wa sekta ya afya ya mkoani hapa uliokuwa ukijadili mkakati wa kupunguza vifo vya wajawazito na watoto wa chini ya miaka mitano.

SERIKALI KUTENGENEZA AJIRA 800,000

SERIKALI imesema katika mwaka huu wa fedha, itatengeneza ajira 800,000 katika fani mbalimbali nchini.
Kauli hiyo ya serikali ilitolewa bungeni jana na Waziri wa Kazi na Ajira, Gaudensia Kabaka, alipokuwa akiwasilisha makadirio ya mapato na matumizi kwa wizara yake kwa mwaka 2012/2013.

Watoto wa mitaani watishia usafi Moshi

HALMASHAURIA ya Manispaa ya Moshi inakabiliwa na ongezeko la watoto wa mitaani wanaotishia kuibuka kwa vitendo vya uhalifu, huku mashirika ya Serikali na yasio ya Serikali yakitakiwa kusaidia kutoa elimu na ajira.
 
Akizungumza mwishoni mwa wiki iliyopita, Mkurugenzi wa Manispaa ya Moshi, Bernadette Kinaboalisema halmashauri ina hofu baada ya ongezekola watoto wa mitaani,hali inayoweza kusababisha kuongezeka kwa vitendo vya ujambazi na magonjwa ya maambukizi. 

Monday 6 August 2012

SA's Keagan wins Big Brother StarGame

 Cape Town - South Africa's Keagan Petersen was announced the winner of AfricaMagic'sBig Brother StarGame on Sunday.

Cape Town-born Keagan, 22, is the first South African to win the competition and competed against housemates Kyle, Lady May, Prezzo, Talia and Wati in the final week. 

Keagan
Keagan walked away the winner after 91 days in the house with a grand prize of $300 000.

According to TVSA, Keagan plans to invest his prize money, help his family and give some to charity. 

Big Brother StarGame was a hit on TV screens generating over 2 million messages to TV and over 250 000 Twitter followers.

MAHAKAMA ZATAKIWA KUHARAKISHA KESI ZA UKATILI DHIDI YA WANAWAKE


NAIBU Waziri wa Sheria na Katiba, Angellah Kairuki, amezitaka mahakama kuharakisha kesi zinazohusu ukatili wa kingono dhidi ya wanawake na watoto, pia amewaonya watu kutokuingilia uhuru wa mahakama.
Kairuki alisema hayo mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam katika uzinduzi wa Mradi wa Haki za Wanawake (HAWA), na kushauri kesi hizo zimalizike ndani ya miezi sita.

GEITA DOCUMENTARY

Contributors