Tuesday 29 March 2011

ZIARA YA MAKAMU WA RAIS WILAYANI MONDULI

 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dk. Mohamed Gharib Bilal, akizungumza na Wanafunzi wa Shule ya Sekondari Engutoto (hawapo pichani) katika Wilaya ya Monduli Mkoani Arusha, wakati alipotembelea Shule hiyo kwa ajili ya kufunguwa Jengo la Bwalo wa Wanafunzi, Makamu Rais yupo Mkoani Arusha kukaguwa na kizinduwa miradi ya maendeleo. katikati Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Monduli Mhe. Edward Lowassa na Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. Isidore Shirima.

 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dk. Mohamed Gharib Bilal katikati, akitembelea mashamba ya kilimo cha mpunga katika mabonde ya Mto wa Mbu Wilayani Monduli, wakati alipokuwa katika siku ya tatu ya ziara yake ya kukaguwa na kuzinduwa miradi ya maendeleo Mkoani Arusha leo. kulia Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe.Isidore Shirima

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dk. Mohamed Gharib Bilal, akiweka jiwe la msingi ujenzi wa jengo la Maabara katika Shule ya Sekondari Nanja Wilayani Monduli, alipokuwa katika mfululizo wa ziara yake ya kukaguwa na kuzinduwa miradi ya maendeleo Wilayani Monduli Mkoani Arusha. kulia Mbunge wa Monduli Mhe.Edward Lowassa na Mkuu wa Mkoa Arusha Mhe. Isidore Shirima.

No comments:

GEITA DOCUMENTARY

Contributors