Monday 28 March 2011

MKASA WA LEO

MKE WA RAIS KUWA RAIS BILA MUME
 

Mke wa rais wa Guatemala ameamua kutengana na mumewe, kwa sababu mke huyo anataka kugombea urais.

Katiba ya Guatemala inapiga marufuku watu wa karibu wa rais kugombea urais. Msemaji wa mahakama ambapo talaka hiyo itashughulikiwa amesema, Edwin Escobar amesema mchakato wa talaka umeanza, kati ya Sandra Torres de Colom na rais Alvaro Colom, ambaye hawezi tena kuwania urais.


Iwapo mume huyo atakubali kutoa talaka, wawili hao watakuwa wametengana rasmi ndai ya kipindi cha mwaka mmoja. Bi Torres alitangaza mapema mwezi huu kuwa atakuwa mgombea urais kupitia chama kinachotawala, katika uchaguzi utakaofanyika mwezi septemba mwaka huu.

Haijafahamika kama akishakuwa rais atarudiana na mumewe, au katiba pia inakataza hilo.

Na kwa taarifa yako.... Kwa wale wanaojua stempu ni nini -- Uingereza ni nchi pekee duniani ambayo stempu zake hazina jila la nchi

1 comment:

Anonymous said...

Hey there! Do you know if they make any plugins to help with SEO?
I'm trying to get my blog to rank for some targeted keywords but I'm not seeing very good gains.
If you know of any please share. Appreciate it!

http://aparmentreviews.webs.com/
Also visit my website : apartment review

GEITA DOCUMENTARY

Contributors