Tuesday 24 December 2013

GEITA MODERN TAARAB NA MKAKATI WA KUISHIKA KANDA YA ZIWA NA TANZANIA KWA UJUMLA.

 Na Steven Mruma [Geita]

   Ilikua ni mazoea ya kawaida sana kuona muziki wa  mwambao kuwika na kushika sana maeneo ya pwani na hasa visiwani Zanzibar, lakini siku hazigandi na muziki wa taarab sasa upo kila mahali na unapendwa na karibu kila mtu, mkoani Geita lipo kundi la muziki wa taarab linaloitwa Geita Modern Taarab, bado ni kundi changa likikabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo kukosa vyombo vya muziki na pesa kwa ajili ya kuanza kurekodi nyimbo zao.
   Kiongozi wa kundi hiloHadija Kabaju alito wito kwa wana Geita na watu wa Kanda ya ziwa kuwaunga mkono na kuwasaidia mambo mbalimbali ili kundi hilo liweze kufikia malengo yake kwa mantiki ya kutoa elimu na burudani ya aina yake na kuweza kuutangaza vizuri mkoa mpya wa Geita,
    Kiongozi huyo alitoa wito huo pamoja na shukrani zake kwa Mh. Vicky Kamata mbunge wa viti maalum Geita kwa kuwapatia msaada wa kinanda ambacho kitasaidia sana kukinyanyua kikundi hicho cha  Muziki wa taarab.
Mh. mbunge viti maalu Geita Vicky Kamata akiwakabidhi kinanda alichowazawadia kikundi cha muziki wa taarab, Geita Modern Taarab
Wanamuziki wa kundi la Geita Modern Taarab wakiwa na kinanda walichozawadiwa na Mh. Vicky Kamata.
Mh. Vicky Kamata akipeana mkono na Kiongozi wa kundi hilo Hadija Kabaju mwenye nguo nyekundu

Geita Modern Taarab
Mh. Vicky Kamata akizungumza na kundi la muziki wa mwambao Geita Modern Taarab

Mh. Vicky ambaye pia ni msanii wa muziki akisisitiza jambo alipokutana na kundi la Geita Modern Taarab,

Bila shaka kila mmoja alikua na furaha.

No comments:

GEITA DOCUMENTARY

Contributors