Wednesday 5 September 2012

MAREHEMU DAUD MWANGOSI AZIKWA KIJIJINI KWAO BUSOKA

Mjane wa marehemu Daud Mwangosi akilia kwa uchungu  juu ya kaburi la mumewe  mara baada ya  mazishi
 MAZISHI ya Mwandishi wa Habari, Daud Mwangosi yalifanyika jana katika Kijiji cha Busoka kilichoko wilayani Rungwe, Mbeya na kuhudhuriwa na mamia ya waombolezaji wakiongozwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Kazi Maalumu), Profesa Mark Mwandosya na Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Willibrod Slaa. 

Katika mazishi hayo, viongozi hao wawili kila mmoja alitangaza kuwasomesha watoto wa marehemu Mwangosi ambaye alifariki dunia Septemba 2, mwaka huu baada ya kupigwa na kitu kinachodhaniwa kuwa ni bomu wakati polisi walipokuwa wakisambaratisha mkutano wa Chadema.

No comments:

GEITA DOCUMENTARY

Contributors