Sunday 2 September 2012

KATIBU WA CCM MKOA WA MOROGORO AFARIKI

Katibu wa CCM mkoa wa Morogoro Bi. Asha Kipangula afariki dunia jana tarehe 1/09/2012 majira ya asubuhi katika hospitali ya TMJ Mikocheni,alipokuwa anauguzwa kutokana na maradhi yatokanayo na kujaa kwa lehemu (Cholesterol).

Mwili wa marehemu umeagwa leo asubuhi saa tatu katika hospitali ya rufaa ya Muhimbili kwa safari ya kwenda mkoani Iringa kwa mazishi.Taarifa zilizopo ni kwamba Mwili wa marehemu utapitishwa katika ofisi za chama mkoani Morogoro kwa ajili ya taratibu ya ndugu,jamaa,viongozi na wanachama wa mkoani hapo kutoa heshima zao za mwisho kwa mpendwa wao kabla ya kuendelea na safari ya kuelekea Iringa baadae mchana.


                "MUNGU AILAZE ROHO YA MAREHEMU MAHALI PEMA PEPONI" 

1 comment:

Anonymous said...

delivers the latest breaking dirt and communication on the latest high point stories, weather, business, spectacular, diplomacy, and more. In the interest in-depth coverage
<a href="http://http://oczyszczanie-organizmu.com.pl>oczyszczanie</a>
[url=http://oczyszczanie-organizmu.com.pl]oczyszczanie[/url]

GEITA DOCUMENTARY

Contributors