Tuesday 24 September 2013

PICHA: TUKIO LA UGAIDI KENYA [WESTGATE MALL] JESHI LAKARIBIA KUDHIBITI MAGAIDI.. VICKY KAMATA BLOG NA VICTORIA FOUNDATION WATOA POLE.


Polisi wakipambana na Magaidi na Mwili wa mmoja wa raia wasio na hatia waliouwawa ukionekana sehemu ya kuingilia
    Mnamo siku ya Jumamosi Kenya ilikumbwa na Balaa la kuvamiwa na akuuwawa watu zaidi ya 50 kwa kupigwa risasi na magaidi wa kikundi cha al shabab katika Super market maarufu kama WESTGATE MALL Jiji Nairobi.
    Msemaji wa jeshi la Kenya kanali Cyrus Oguna alisema jumapili usiku kwamba jeshi hivi sasa linadhibiti kabisa soko la maduka ya kifahari mjini Nairobi  la Westgate Mall ambako watu 68 waliuwawa na wanamgambo wa kisomali wa kundi la Al-shabab.
mmoja wa majeruhi akpatiwa huduma
Anasema wengi wa mateka waliokuwa wamezuiwa ndani ya soko hilo kubwa wameokolewa lakini inavyoonekana washambuliaji wangali wanawashikiliwa mateka katika sehemu ya maduka na Jeshi la ulinzi la Kenya KDF linadhibiti jengo zima.  Anasema idadi ya watu wanaoshikiliwa mateka haijazidi 10.

Uvamizi wa jengo hilo unaingia katika siku ya tatu jumatatu na jeshi linakadiria kuna kati ya washambuliaji 10 hadi 15.

Wanamgambo wa kundi la Kisomali la Al-Shabab wamedai kuhusika na shambulio hilo na kutishia jumatatu asubuhi kwamba watawauwa mateka wote ikiwa jeshi litaendelea kuwashambulia.

Shambulio hilo lilianza takriban saa sita mchana kwa saa za Kenya  siku ya jumamosi katika soko la maduka ya kifahari la Westgate Mall na kusababisha vifo vya watu 68 na takriban 175 kujeruhiwa kufuatana na maafisa wa serikali.
      Akilihutubia taifa Rais Uhuru Kenyatta katika hotuba yake kwa hamasa aliapa  kusimama imara kupambana na kitisho cha ugaidi  akiongeza kusema kwamba vikosi vya usalama vya Kenya vina nafasi nzuri ya kuwashinda waliohusika na shambulio hilo.
Rais wa Kenya Uhuru Kenyata.
 Akizungumza na Sauti ya Amerika-VOA mchambuzi wa masuala ya kiusalama na kijeshi Godwin Chilewa anasema huwenda kulikuwa na kasoro katika mfumo kamili wa usalama wa Kenya lakini ni vigumu kwa wakati huu kuvilaumu vikosi vya usalama hadi uchunguzi kufanyika.
  Anasema tatizo kuu linaweza kuwa ni ukosefu wa mawasiliano kati ya idara mbali mbali za usalama na namna ya kukusanya habari za kijasusi na jukumu la raia vile vile.

Rais Barack Obama amezungumza na kiongozi mwenzake Uhuru Kenyatta na kutoa rambi rambi zake na kuahidi uungaji mkono wa Marekani katika juhudi za Kenya kupambana na ugaidi.

    "VICKY KAMATA BLOG NA VICTORIA FOUNDATION WANAWAPA POLE WALE WOTE WALIOPOTEZA NDUGU ZAO NA PIA INAWAPA POLE NA KUWAOMBEA WAHANGA WA TUKIO HILO KWA UJUMLA,LAKINI PIA INAWAOMBEA WALIOJERUHIWA KATIKA TUKIO HILO LA UGAIDI WAPONE HARAKA.

     VICTORIA FOUNDATION NA VICKY KAMATA BLOG KWA UJUMLA INALAANI KITENDO HICHO CHA KINYAMA KWA RAIA WASIO NA HATIA. 

   PIA TUZIDI KUIOMBEA NCHI YETU MUNGU AKAIEPUSHE NA MAJANGA KAMA HAYA AMBAYO YANACHUKUA ROHO ZA WATU WASIO NA HATIA NA KUONDOA NGUVU KAZI YA TAIFA KWA UJUMLA".


PICHA ZA TUKIO HILO, NA JINSI WANAJESHI POLISI KENYA WAKISHIRIKIANA NA MAKOMANDOO WA MAREKANI NA ISRAELI KUWADHIBITI MAGAIDI WALIOPO NDANI


Majeruhi akiwahishwa hospitali
Majeruhi akioka katika jengo akiwa amejeruhiwa vibaya
Maofisa uslama wakipambana na magaidi ndani ya WESTGATE MALL
Mauaji ya kinyama yaliyofanywa na Magaidi wa kikundi cha Al-shabab
Majeruhi akpatiwa huduma [akipandishwa kwenye ambulance]
mwili wa mmoja wa raia wasio na hatia waliouwawa na magaidi
Magaidi wa kikundi cha al-shabab wakionekana ndani ya jengo hilo wakiendelea kushikilia mateka na kuua watu wasio na hatia


Wahanga wa tukio hilo wakikimbia kunusuru maisha yao na pembeni ukionekana mwili wa mtu aliyeuwawa na magaidi hao
Majeruhi akiwahishwa hospitali
Wanajeshi wakiwa tayari kwa mapambano ndani ya jengo waliopo magaidi wa al-shabab
Hali inatisha ndani ya Jengo la WESTGATE MALL ni machozi na damu
Mwili wa mtu aliyeuwawa ukionekana ndani ya jengo la westgate mall.
Ulinzi usiku na mchana kuhakikisha magaidi hao wanatiwa mbaroni.
Jengo la westgate mall lifuka moshi wakati wa mapambano kati ya maofisa wa usalama na magaidi
Majeruhi akisaidiwa
majeruhi
Mama akiwa na watoto wake waliamua kujificha kwa style hii kuokoa maisha yao
Sehemu ya mgahawa ambao pia ulishambuliwa vikali na magaidi
Rai waliokuwa mateka wakitoka nje ya jengo baada ya kuokolewa na vikosi vya usalama
Wanausalama wakiwa kazini kupambana na magaidi  na mwili wa raia aliyeuwawa na magaidi hao wa al-shabab
Majeruhi akipandishwa kwenye ambulance
Baadhi ya raia waliokuwa wameshikiliwa mateka wakitoka baada ya kuokolewa.



Eneo la maegesho ya magari ikionekana miili ya watu waliouwawa na wengine wakiomba msada kwa ishara ya kujisalimisha.
Rais wa Kenya Uhuru Kenyata akioa salamu za rambirambi kwa wahanga na pia kuzungumzia tukio hilo kwa ujumla.
Raia wakikimbia kutoka nadni ya jengo baada ya kuokolewa na vikosi vya usalama.
Wanajeshi wakiwa tayari kwa mapambno nje ya jengo
Wanajeshi wa kenya wakizidi kujipenyeza ndani ya jengo hilo kupambana na magaidi hao wa al-shabab.

No comments:

GEITA DOCUMENTARY

Contributors