Wednesday 25 September 2013

WANANCHI WA JIMBO LA GEITA, WANUFAIKA NA MRADI WA SOLAR [UMEME WA JUA] WENYE THAMANI YA TSH. MILIONI 293 ULIOFADHILIWA NA MBUNGE WAO VICKY KAMATA.

      Wanachi wa jimbo la Geita mkoa mpya wa Geita Wanufaika na Mradi wa Solar Uliofadhiliwa na Mbunge wa viti maalum Geita Mh. Vicky Kamata wenye Thamani ya Shilingi Milioni 293.   Mradi huo umewafikia wananchi wote wa kata zote za jimbo la Geita.
      Akizungumzia ufadili huo Vicky Kamata amesema Solar zitasaidia kuboresha huduma za afya na Elimu Jimboni hapo, kwani changamoto ya kukosa umeme ilikua inarudisha nyuma maendeleo ya Jimbo hilo. "Angalau sasa wanachi wa Geita watanufaika na ufadhili huo katika secta ya afya na Elimu ambao ndio nguzo kuu za maendeleo", alisema Mh. Vicky katika Hafla ya Kufunga Solar hizo iliyo hudhuliwa pia na mkuu wa wilaya ya Geita Mh. Manzie Mangochie ambaye alikuwa mgeni rasmi.
     Maeneo yaliyofungwa Solar ni Zahanati zote za jimbo la Geita na Nyumba za watumishi wa Afya pamoja na nyumba za baadhi ya Walimu na Shule za sekondari na chache za Msingi. 

Maeneo yaliyonufaika na ufadhili huu ni kama ifuatavyo:-

  •     Kwa upande wa AFYA kata zilizo nufaika na na ufadhili huo ni 

  1. Kata ya Nzela,- Kituo cha afya Nzela majengo nane [8] ya zahanati yalipata solar na nyumba nne [4] za waatumishi wa afya pia zilipata Solar
  2. kata ya Bugulula - Kituo cha afya Kasota Jengo moja [1] lilipata solar na nyumba mbili [2] za watumishi wa afya.
  3. Kata ya Bulela - Kituo cha afya  Bulela Jengo Moja [1]  lilipata solar  na nyumba mbili [2] za watumishi wa afya.
  4. Kata ya Lubanga - kituo cha afya Lubanga jengo moja [1] lilipata solar   na nyumba moja [1] ya mtumishi wa afya.
  5. Kata ya Nkome - kituo cha afya Nkome jengo moja [1] lilipata solar .
  6. Kata ya Senga - kituo cha afya Senga jengo moja [1] lilipata solar na nyumba mbili [2] za watumishi wa afya.
  7. Kata ya Lwenzela - Kituo cha afya Lwenzela jengo moja [1] lilipata solar na nyumba mbili [2] za watumishi wa afya.
  8. Kata ya Bugulula - Kituo cha afya Bugulula jengo moja [1] lilipata solar na nyumba moja [1] ya mtumishi wa afya.
  9. Kata ya Isulwa Butumbwe - kituo cha afya Kifufu jengo moja [1] lilipata solar na nyumba moja [1] ya mtumishi wa afya.
  10. Kata ya Bung`wangoko - kituo cha afya Nyakaduha jengo moja [1] lilipata solar na kituo cha afya cha Kishinda jengo moja [1]
  •   Kwa Upande wa Elimu maeneo yaliyonufaika ni kama ifuatavyo:-

  1. Kata ya Kakubilo - Shule ya Sekondari Kikubilo Solar Moja [1] na nyumba moja [1] ya mwalimu ilipata solar.
  2. Kata ya Bugalama - shule ya Shule ya Sekondari Bugalama solar Moja [1] na solar katika nyumba mbili [2] za walimu pia zilipata solar
  3. Kata ya Bung`wangoko- Bung`wangoko Sekondari Solar moja [1]. 
  4. Kata ya Katoma - Shule ya sekondari Katoma solar moja [1] na Shule ya sekondari Nyamboge solar moja [1].
  5. Kata ya Nyanguku - Shule ya sekondari Nyanguku Solar moja [1].
  6. Kata ya Kagu  - Shule ya sekondari Kagu Solar moja [1] na Nyumba mbili [2] za walimu zilipata solar pia Shule ya msingi Nyawilimilwa walipata Solar moja [1] na nyumba mbili [2] za walimu pia zilipata solar.
    Katika Kata za Kasamwa, Mtakuja na Karangalala Zipo katika Gridi ya taifa ya ememe na hivyo kuwa na uhakika wa kupata umeme kutoka katika Gridi ya Taifa.

Baadhi ya picha katika tukio la uzinduzi na ufungwaji wa solar jimboni Geita.

Mkuu wa wilaya ya Geita Mh. Manzie Mangochie akizindua mradi kwa kuweka jiwe la msingi la mradi huo [jiwe la msingi halionekani pichani] pamoja na Mbunge wa viti maalum Geita Mh. Vicky Kamata.
Viongozi mbalimbali wa chama na serikali pamoja na wananchi wakiambatana na mfadhili wa Solar ambae pia ni Mbunge wa viti maalum Geita Mh. Vicky Kamata walihudhuria ufungwaji huo wa solar
 
Mitambo ya kisasa ikiwa imefungwa kataka kituo cha afya Nzela.
Mh. Vicky Kamata Mbungewa viti maalum Geita akifatilia kwa ukaribu ufungwaji wa solar na nyuma ni Katibu msaidizi wa CCM wilaya ya Geita Bwana Kusaga.

Mitambo Solar system ya kisasa iliyofadhiliwa na Mh. Vicky Kamata ambaye ni Mbunge wa viti maalum Geita.

Baadhi ya Solar zilizofadhiliwa  na Mbunge wa viti maalum Geita Mh. Vicky Kamata.

Mafundi wa Solar wakifunga solar katika Moja ya Zahanati.

Baadhi ya wananchi hawakuwa nyuma walifuatilia kwa ukaribu ufungwaji wa Solar hizo popote pale walipokuwa na uwezo wa kufika.

No comments:

GEITA DOCUMENTARY

Contributors