Friday 27 September 2013

MAKAMU WA PILI WA RAIS ZANZIBAR MHE. BALOZI SEIF ALI IDDI AZINDUACHAPISHO LA MGAWANYO WA IDADI YA WATU KWA UMRI NA JINSI.

    Makamu wa pili wa rais Zanzibar Mh. Balozi Seif Ali Iddi (Mb na MBW) Amezindua chapisho la mgawanyo wa idadi ya watu kwa umri na jinsi katika ukumbi wa kimataifa wa mikutano wa Mwl. Julius Nyerere Jijini Dar es salaam siku ya tarehe 25 september 2013.
   Akizindua chapisho hilo Mh. Balozi Seif Iddi Alisema""
Serikali  zote Nchini zitaendelea kushirikiana na washirika wa maendeleo ndani na nje ya nchi kupitia mipango ya maendeleo ziliyo jiwekea ya Dira ya Taifa ya Maendeleo 2025 na  Mpango wa kupunguza umaskini { Mkuza } katika kuimarisha Sekta ya Elimu, Afya na soko la ajira ili kuweza kukabiliana na kasi ya ongezeko la idadi ya watu hapa Nchini.  Mwenyekiti huyo Mwenza wa Kamati Kuu ya Taifa ya Sensa ya Watu na Makazi Tanzania Balozi Seif Ali Iddi alisema hayo wakati  akizindua chapisho la mgawanyo wa idadi ya watu kwa umri na jinsi kwenye sensa ya watu na makazi ya mwaka 2012 hafla iliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere Jijini Dar es salaam.
 Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Balozi Seif Ali Iddi ambaye pia ni Mwenyekiti mwenza wa Kamati Kuu ya Taifa ya Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka 2012, akiwakabidhi baadhi ya viongozi na wananchi vitabu vya machapisho ya mgawanyo wa watu kwa umri na jinsi mara baada ya kuzindua rasmi chapisho hilo kwenye ukumbi wa kimataifa wa mwalimu Nyerere jijini Dar es salaam. Anaye kabidhiwa ni M/kiti wa uchumi viwanda na Biashara Mh. Mahmudu mgimwa akishuhudiwa na Hajatt Amina M, Said wa pili kutoka kushoto na kulia ni Naibu waziri wa Fedha Saada Mkuya.
Viongozi mbalimbali wa serikali na wadau wa mashirika mbalimbali wakiwa katika picha ya pamoja katika uzinduzi wa chapisho la mgawanyo wa idadi ya watu kwa umri na jinsi uliofanyika katika ukumbi wa kimataifa wa mikutano wa Mwl. Julius Nyerere jijini Dar es saalam.

Naibu waziri wa Fedha Saada Mkuya akitoa hotuba katika uzinduzi huo.
Baadhi ya Wabunge wakifuatilia kwa umakini uzinduzi huo. kutoka kulia ni Mh.Vicky Kamata, Mh. Paul Kimiti, Mh, Mustafa Mkulo na Mh. Sophia Simba.
Mgeni Rasmi wa uzinduzi wa chapisho la mgawanyo wa idadi ya watu kwa umri na jinsi Mh. Balozi Seif Ali Iddi akimkabidhi mwenyekiti wa uchumi viwanda na biashara Mh. Mahamudu Mgimwa chapisho hilona nyuma kulia ni Naibu waziri wa fedha Mh, Saada Mkuya.
Mgeni Rasmi wa uzinduzi wa chapisho la mgawanyo wa idadi ya watu kwa umri na jinsi Mh. Balozi Seif Ali Iddi akimgawa chapisho la mgawanyo wa idadi ya watu kwa umri na jinsi.
Mgeni Rasmi wa uzinduzi wa chapisho la mgawanyo wa idadi ya watu kwa umri na jinsi Mh. Balozi Seif Ali Iddi akimgawa chapisho la mgawanyo wa idadi ya watu kwa umri na jinsi kwa viongozi, wawakilishi wa mashirika mbalimbali na wananchi.

2 comments:

Anonymous said...

order tramadol buy tramadol no prescription cod - tramadol 50 mg with alcohol

Anonymous said...

Very nice!
http://pnck92x2.com

GEITA DOCUMENTARY

Contributors