Saturday 11 March 2017

VICTORIA FOUNDATION YAGAWA MASHUKA 100 HOSPITAL YA MKOA WA GEITA


Tarehe 10.03.2017
Mhe Vicky Kamata Likwelile Mbunge wa viti maalum Mkoa wa Geita amefanya ziara na kugawa mashuka 100 katika hospitali ya Mkoa wa Geita kwenye ward ya akina mama na watoto,
Aidha Mhe Vicky Kamata Likwelile amesikiliza changamoto mbalimbali za wagonjwa ikiwemo tatizo la upungufu wa vitanda pamoja na ward za akinamama.
Lakini pia amesikiliza changamoto mbalimbali toka kwa watumishi wa hospital hiyo ikiwemo suala la uchache wa wahudumu wa afya na Madaktari ikiwemo madaktari wa magonjwa ya akina mama na watoto.
Mhe Vicky Kamata Likwelile ameahidi kuzifanyia kazi changamoto hizo.
Katika ziara hiyo ya Mhe Vicky Kamata Likwelile aliambatana na viongozi wa wa UWT akiwemo Mhe Maimuna Mingisi (DV) Mwenyekiti wa UWT Mkoa wa Geita na Ndugu Mazoea Salum Katibu wa UWT Wilaya ya Geita.
Mhe Vicky Kamata amewashukuru madaktari na wauguzi wa Hospitali hiyo na kuwapongeza kwa kazi nzuri wanazofanya za kuwahudumia wagonjwa.
Imetolewa na
Mazoea Salum
Katibu wa UWT
Wilaya ya Geita
Imehaririwa na Steven Mruma Jr.






No comments:

GEITA DOCUMENTARY

Contributors