Monday 26 November 2012

BREAKING NEWS: SHARO MILIONEA AFARIKI DUNIA


HABARI ZISIZOTHIBITISHWA ZILIZOTUFIKIA HIVI PUNDE: Msanii mahiri wa uchekeshaji na mwanamuziki wa Bongo Fleva Sharo Millionea amefariki katika ajali ya gari huko Muheza mkoani Tanga. Tutaendelea kuwajulisha kadiri tutakavyopata habari zaidi.

ALICHOKISEMA KAMANDA WA POLISI MKOA WA TANGA
Kuhusu kifo cha msanii/mwigizaji Sharo Milionea, namkariri Kamanda wa Polisi Tanga akisema “leo majira ya saa mbili usiku kwenye barabara ya Segera Muheza mtu mmoja alietambulika kwa jina la Hussein Ramadhani au Sharo Milionea akiwa anaendesha gari namba T478 BVR Toyota Harrier akitokea Dar es salaam kwenda Muheza alipofika eneo hilo gari lake liliacha njia na kupinduka mara kadhaa na kusababisha kifo chake, mwili wa marehemu umehifadhiwa kwenye hospitali Teule ya wilaya ya Muheza”
Kamanda amesema hakuna kona kali sana wala ubovu wa barabara kwenye sehemu aliyopata ajali Sharo Milionea, katikati ya Segera na Muheza ambapo gari imehifadhiwa mahali salama kwa sababu haitembei.
Kwenye gari alikua mwenyewe. 

No comments:

GEITA DOCUMENTARY

Contributors