Wednesday, 21 August 2013

RAIS JAKAYA KIKWETE AFANYA MABADILIKO YA MAKATIBU WAKUU NA MANAIBU WAKE..

RAIS J.M. KIKWETE
     RAIS Jakaya Kikwete amefanya mabadiliko ya uongozi katika ngazi za juu za utendaji wa Serikalini kwenye nafasi za Makatibu Wakuu na Naibu Makatibu Wakuu katika Wizara mbalimbali, ambapo  wapo waliohamishwa, wataopangiwa kazi nyingine na yumo anayestaafu.

Kauli hiyo ilitolewa leo jioni na Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue wakati akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam.

“Rais amefanya mbadiliko haya kwa lengo kuu la kuimarisha utendaji wa kazi za Serikali katika ngazi hizo za juu,” alisema Balozi Sefue.

Mabadiliko yaliyofanywa kwa upande wa Makatibu Wakuu ni kama ifuatavyo:

Katibu mkuu kiongozzi Balozi OMBENI SEFUE
  • Dk Florens Turuka amekuwa Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu, awali alikuwa Katibu Mkuu Wizara ya Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia.

  • Joyce Mapunjo amekuwa Katibu Mkuu Wizara ya Ushirikiano wa Afrika Mashariki, awali alikuwa Katibu Mkuu Wizara  ya Viwanda, Biashara na Masoko.

  • Jumanne Sagini amekuwa Katibu  Mkuu  Ofisi ya Waziri Mkuu - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) awali alikuwa Naibu Katibu  Ofisi wa Waziri Mkuu - TAMISEMI.

  • Dk Servacius Likwalile amekuwa Katibu Mkuu Wizara ya Fedha, awali alikuwa Naibu Katibu Wizara ya

Fedha.

  • Dk Patrick Makungu amekuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, awali alikuwa  Naibu Katibu Mkuu katika Wizara hiyo.

  • Alphayo Kitanda amekuwa Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, awali alikuwa Naibu Katibu Ofisi ya Waziri Mkuu – TAMISEMI.

  • Dk Shaaban Mwinjaka amekuwa Katibu Mkuu Wizara ya Uchukuzi, awali alikuwa Naibu Katibu Mkuu Wizara  ya Viwanda, Biashara na Masoko.

  • Dk Uledi Mussa amekuwa Katibu Mkuu Wizara  ya Viwanda, Biashara na Masoko, awali alikuwa Wizara ya Ushirikiano wa Afrika Mashariki. 

  • Profesa Sifuni Mchome amekuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya  Elimu na Mafunzo ya Ufundi, awali alikuwa Katibu Mtendaji Mkuu wa Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania.

  • Charles Pallangyo amekuwa Katibu Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, awali alikuwa Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri.

  • Anna Maembe amekuwa Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto, awali  alikuwa Naibu Katibu Mkuu wizara hiyo.

  • Sihaba Nkinga amekuwa Katibu  Mkuu wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, awali alikuwa Naibu Katibu Mkuu Wizara hiyo.

  • Sophia Kaduma amekuwa Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo, Chakula na Ushirika, awali alikuwa Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo.

Balozi Sefue aliongeza kwamba:

  • Katibu Mkuu aliyepewa uhamisho ni  Peniel  Lyimo ambaye anahamia Ofisi ya Rais - Ikulu  kwenye “Presidential’s Delivery Bureau” kama Naibu Mtendaji Mkuu mwenye jukumu la kuanzisha na kuongoza Idara ya Mageuzi ya Kilimo mwanzoni alikuwa  Katibu Mkuu  Ofisi ya Waziri Mkuu.

Makatibu wakuu watakaopangiwa kazi nyingine ni:-

  • Sethi Kamuhanda aliyekuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo 

Sunday, 18 August 2013

VIONGOZI SADC WAMPIGIA SALUTI RAIS KIKWETE, "JOYCE BANDA NAE ANENA"ATAKA WANWAKE WAPEWE NAFASI"

Baadhi ya wakuu wa SADC

           RAIS wa Malawi, Joyce Banda amempongeza Rais Jakaya Kikwete kwa kuimarisha demokrasia, amani na usalama katika nchi za Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za kusini mwa Afrika (SADC).
           Banda alitoa pongezi hizo wakati akihutubia Mkutano wa 33 wa Wakuu wa SADC baada ya kukabidhiwa nafasi ya uenyekiti wa jumuiya hiyo kutoka kwa Rais wa Msumbiji, Dk Armando Guebuza.
        “Wananchi wa Malawi, mimi na SADC tunampongeza Kikwete kwa kuimarisha amani, demokrasia na usalama katika jumuiya katika kipindi chake cha uongozi (wa Asasi ya Siasa,Ulinzi na usalama “Pia Rais wa Msumbiji, Armando Guebuza katika uongozi wake wa uenyekiti alishirikiana na Kikwete kushughulikia matatizo ya kisiasa na kuufanya ukanda wa nchi za SADC kuwa na amani,” alisema Rais Banda, ambaye nchi yake ina mgogoro na Tanzania upand wa ziwa Nyasa.
        
Rais Kikwete na Rais Joyce Banda wa Malawi
  Mgogoro huo uliibuka baada ya Serikali ya Malawi bila kushauriana na Tanzania, kutoa leseni kwa kampuni mbili za kigeni, kutafuta mafuta katika eneo la Ziwa upande wa Tanzania na kuibua mgogoro huo.
       Chanzo cha mgogoro huo unaoshughulikiwa na jopo la marais wastaafu wa Afrika; Thabo Mbeki (Afrika Kusini), Joachim Chisano (Msumbiji), Festus Mogae (Botswana) na wanasheria saba wa kimataifa, ni mikataba yenye utata iliyoachwa na wakoloni. Alisema ambao ndo waloigawa mipaka hiyo wakati wa ukoloni.
       Katika kipindi cha mwaka mmoja cha uongozi wa Rais Kikwete katika asasi hiyo ya siasa, ulinzi na usalama aliweza kufanikisha kufanyika kwa uchaguzi mkuu wa Zimbabwe, ambao Robert Mugabe ameshinda kuingoza nchi hiyo kwa muhula mwingine na kumbwaga mpinzani wake mkubwa na aliyekuwa waziri mkuu Morgan Tvshangirai.
      Amefanikisha pia kuanza kwa mchakato wa amani na kuatikana kwa muafaka wa kisiasa nchini Madagascar.
    Pia katika kipindi chake, alifanikisha kupelekwa kwa wanajeshi wa kulinda amani katika mji wa Goma, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) ambapo waasi wa M23 wanapambana na wanajeshi wa serikali. Wanajeshi hao wa kulinda amani wametoka Tanzania, Malawi na Afrika Kusini.

        Rais Kikwete amekabidhi madaraka hayo jana kwa Rais wa Namibia, Hifikepunye Pohamba. Rais huyo wa Malawi Bi. Joce  Banda ameahidi amani, Akizungumzia mkakati wake wakati wa uongozi wake wa mwaka mmoja kama Mwenyekiti wa SADC, Banda alisema ili ukanda wa SADC uwe na amani na usalama ni lazima nchi wanachama zipambane na umasikini.

       “Lazima tuimarishe siasa za ndani za nchi zetu, tuwe wavumilivu wa kisiasa na tusaidie wanawake wasiwe nyuma,” alisema. Aliahidi kuimarisha jumuiya za kikanda pamoja na kilimo kwa maelezo kuwa kilimo ndicho mwajiri mkuu wa wananchi wa nchi za SADC.
“Nitahamasisha kilimo kiboreshwe ili wananchi wa SADC waweze kuendesha kilimo cha biashara na pia sekta binafsi waingie kwenye kilimo na tupate masoko mapya ya bidhaa za kilimo nje ya mipaka ya ukanda wetu”.
      Alitaka katika ukanda wa jumuiya ya SADC kuboreshwe mwingiliano wa wananchi wa nchi za ukanda huo. Alisema haiwezekani kuboreshwa kwa jumuiya za kikanda bila kuruhusu mwingiliano huru wa wananchi wake.
     Rais Banda alitaka wanawake wapewe nafasi katika uongozi na kujengewa uwezo katika kuimarisha uchumi na kuondokana na umasikini na kusisitiza kuwa, “wanawake ndiyo wanaopambana na umasikini, wanabakwa, wanakabiliwa na unyanyasaji na wengi wamepoteza utu wao”.

      Kwa upande wa Mwenyekiti wa Kamisheni ya Umoja wa Afrika (AU), Dk Nkosazana Dlamini- Zuma alizitaka nchi za Afrika kuimarisha miundombinu ili mazao ya wakulima yaweze kusafirishwa pamoja na kuboreshwa kilimo, uwekezaji na kujengwa kwa viwanda.“Lazima tufanye kazi pamoja kuwahakikishia chakula watu wetu wa SADC na Afrika haiwezi kuendelea bila kuweka wanawake kila maeneo na kutafuta ufumbuzi wa changamoto zinazotukabili za tatizo la ajira kwa vijana, umasikini, sekta duni ya viwanda na tatizo la kutokuwepo usawa wa kijinsia,” alisema Zuma.



Wednesday, 14 August 2013

NECTA: MITIHANI KUSAHIHISHWA KWA COMPUTER, ITAONGEZA UBORA WA USAHIHISHWAJI.



Joyce Ndalichako

          Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani la Taifa (Necta), Dk Joyce Ndalichako amesema baraza lake linajiandaa kutumia teknolojia ya kompyuta wakati wa kusahihisha maswali ya mitihani ambayo wanafunzi wanajibu kwa kujieleza.
Kwa sasa teknolojia ya usahihishaji kwa kompyuta inayotumika nchini ni ile ya kujibu maswali ya kuchagua tu ya`Optical Mark Reader’ (OMR) iliyoanza kutumika mwaka jana kusahihisha mitihani ya darasa la saba.
     
Akizungumza na mwandishi wa habari jana wakati wa Mkutano wa Mabaraza ya Mitihani Afrika (AEAA), unaoendelea mjini hapa, Dk Ndalichako alisema: “Kwa kuanzia, Necta itafanya majaribio ya teknolojia hiyo mwakani na ninaamini itaongeza ubora katika usahihishaji.”
“Kwa kutumia hii teknolojia msahihishaji hawezi kuona namba ya mwanafunzi, anachoona ni sehemu ya swali anayotakiwa kusahihisha na jibu lake, akimaliza swali moja jingine linakuja moja kwa moja,” aliongeza.
   Alisema kwa kutumia teknolojia hiyo, mratibu wa usahihishaji anaweza kuona kazi inayofanywa na msahihishaji yeyote na hata kuwapima kama atakuwa na wasiwasi wowote.
    Alisema Zimbabwe imeanza kutumia teknolojia hiyo aliyosema itasaidia kuongeza ubora katika suala la usahihishaji.
     Akizungumza na waandishi wa habari wakati wa ufunguzi wa mkutano huo jana, alisema teknolojia ya OMR imeongeza ubora wa hali ya juu kwenye mtihani wa darasa la saba pamoja na usahihishaji wake.
“ Watu wanasema kuwa mtihani wa maswali ya kuchagua ni mrahisi, lakini hii siyo kweli, inatungwa na wataalamu na inalenga kumpima mtoto katika kila nyanja, ndiyo maana hata mtihani wa darasa la saba mwaka jana ilibidi Serikali ishushe alama za kwenda kidato cha kwanza zikawa 70 badala ya 100,” alisema Dk Ndalichako.
        Akizungumzia teknolojia hiyo, Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Philipo Mulugo alisema wamebaini kuwa zaidi ya asilimia 80 ya nchi za Afrika zinatumia mfumo wa usahihishaji kwa OMR.
    Alisema baadhi ya nchi zimeanza kusahihisha kwa kutumia kompyuta hata katika maswali ya kujieleza na kuwataka Watanzania kuacha kujirudisha nyuma.

Sunday, 11 August 2013

Mh. VICKY KAMATA NA VICTORIA FOUNDATION KWA UJUMLA WAWAPONGEZA WAISLAM DUNIANI KOTE

Mh. Vicky Kamata
 Familia ya Mh. Vicky Kamata
     Ikiwa ni siku moja baada ya sikukuu ya IDI el fitri Familia ya  Mh. Vicky Kamata ambaye pia ni mbunge wa viti maalum Geita pamoja na Mfuko wake wa VICTORIA FOUNDATION, wamewapongeza waislamu wote duniani kwa kusheherekea sikukuu ya IDI EL FITRI kwa amani na utulivu.  Akitoa pongezi hizo Mh. Vicky alisema "huu ni mfano wa kuigwa katika kila sikukuu ili kuweza kulinda amani ya taifa na Dunia kwa ujumla.."   
        Waislamu wote duniani siku ya Ijumaa na Jumamosi walisheherekea sikukuu hiyo baada ya kumaliza mfungo wa mwezi mtukufu wa Ramadhani.. sikukuu hiyo huadhimishwa na waislamu wote duniani kila mwaka na huendana na mwandamo wa mwezi...


MAMA TUNU PINDA ALIPOTEMBELEA WANAKIJIJI WA ZEGERO

Hivi karibuni mke wa Waziri mkuu Mama Tunu Pinda aliwatembelea wanakijiji wa kijiji cha Zegero ambapo alikutana na viongozi wa serikali ya kijiji akiwemo mwenyekiti, mtendaji wa kijiji na wajumbe...
   katika ziara hiyo aliambatana na Mh. Vicky Kamata Mbunge Viti Maalum Geita,, Officer Mohamedi Mapunda Wa Jeshi la Polisi Makao Makuu na Afisa Kilimo na Mifugo wa Mh. Vicky Kamata Dr. Steven Mruma.. 

                    YAFUATAYO NI MATUKIO MUHIMU YA ZIARA HIYO KATIKA PICHA..
Mama Tunu Pinda akiwa na baadhi ya viongozi wa kijiji cha zegero na mh. Vicky Kamata walipotembelea wanakijiji hao.
Mama Tunu Pinda akisisitiza jambo mbele ya baadhi ya viongozi wa kijiji
Mama Tunu Pinda akifuatilia jambo na Mh. Vicky Kamata Na moja kati ya maofisa wa polisi inspecta Mohamedi Mapunda kulia
Mh. Vicky Kamata akishauri jambo mbele ya Mama Tunu Pinda na Officer M. Mapunda
officer Mohamedi Mapunda akishauri jambo
Mama Tunu Pinda akisalimiana na mmoja ya wanakijiji bwana Susatule..
Mama Tunu Pinda katika Picha ya pamoja na Afisa Kilimo na Mifugo wa Mh. Vicky Kamata Dr. Steven Mruma katikati na kulia ni Mh. Vicky Kamata
Mama Tunu Pinda na Baadhi ya Wajumbe wa Serikali ya kijiji
Mama Tunu PInda akirejea katka ofisi ya kijiji baada ya kukagua miradi mbalimbali ya wanakijiji..
Hapa akiwa na moja ya familia inayoishi Zegero
Akiwa nje ya hema ambalo pia ni moja kati ya sehemu ya malazi ya moja ya wanakijiji
 


akikagua moja ya hifadhi ya misitu ya kijiji hicho..

Monday, 8 July 2013

VICKY KAMATA CUP IKIPAMBA MOTO MKOANI GEITA

             Mheshimiwa Vicky Kamata akiwa na mkuu wa mkoa wa Geita wakati mashindano yakiendelea  
                               Mashabiki wakiwa wamefurika vibaya mno katika viwanja hivyo
             

GEITA DOCUMENTARY

Contributors