Thursday, 12 April 2012
Wizi wa kazi za wasanii waibua mjadala Bungeni
SUALA la wizi wa kazi za wasanii nchini, limeibua mjadala mkali bungeni huku Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Kabwe Zitto akipendekeza mtu atakayekamatwa akiuza CD na DvD feki za kazi za wasanii atozwe faini isiyopungua sh50 milioni.
Mbunge huyo ambaye pia ni Naibu Msemaji wa Kambi rasmi ya upinzani Bungeni, alipendekeza kuwa mtu yeyote atakayekutwa na kazi feki za wasanii naye aadhibiwe vikali ili kujenga Utamaduni wa Watanzania kuacha kununua kazi za wizi wasaniii.
Wabunge hao walichachamaa Bungeni mjini Dodoma jana wakati wakichangia hotuba ya Waziri wa Viwanda na Biashara, Dk. Cyril Chami kuhusu muswada wa sheria ya marekebisho ya sheria mbalimbali za biashara wa mwaka 2011.
Mutharika kuzikwa April 23
IKULU ya Malawi imethibitisha jana kuwa mazishi ya Rais wake wa tatu, Bingu wa Mutharika yatafanyika Aprili 23, mwaka huu katika shamba lake lililopo Ndata, Wilaya ya Thyolo, kusini mwa Mji wa Blantyre.
Uamuzi huo unakwenda sambamba na ule wa kuongezwa kwa siku za maombolezo kutoka 10 hadi 30, ili kuyapa maombolezo hayo uzito unaolingana na msiba wa “mkuu wa nchi aliyefariki dunia akiwa madarakani.”
Uamuzi huo unakwenda sambamba na ule wa kuongezwa kwa siku za maombolezo kutoka 10 hadi 30, ili kuyapa maombolezo hayo uzito unaolingana na msiba wa “mkuu wa nchi aliyefariki dunia akiwa madarakani.”
Awali, kabla ya Rais Banda kuapishwa, Ofisi ya Rais na Baraza la Mawaziri (OPC) ya Malawi, ilitoa taarifa kwamba kungekuwa na siku 10 tu za maombolezo ambazo zilitarajiwa kumalizika Jumapili wiki hii.
Lakini kutokana na kuongezeka kwa siku 20 zaidi, maombolezo hayo yanatarajiwa kukoma ifikapo Mei 6, mwaka huu na katika kipindi chote hicho, bendera zitaendelea kupepea nusu mlingoti huku televisheni na redio zikipiga muziki wa maombolezo.
Wednesday, 11 April 2012
Jenerali Mwita Kyaro afariki dunia
MKUU wa Majeshi Mstaafu Jenerali Ernest Mwita Kyaro, amefariki dunia katika Hospitali ya Bugando jijini Mwanza.
Msemaji wa Jeshi la Wananchi Tanzania ( JWTZ), Kanali Kapambala Mgawe alithibitisha kutokea kwa kifo hicho akieleza kuwa Jenerali Mwita Kyaro alifariki dunia saa 4 asubuhi jana katika hospitali ya Bugando alipokuwa akitibiwa.
Akieleza wasifu wa marehemu huyo, Mgawe alisema Jenerali Kyaro aliongoza jeshi hilo akiwa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama (CDF) kati ya mwaka 1988 hadi 1994 alipostaafu.
“Jenerali Kyaro alistaafu akiwa amelitumikia jeshi kwa miaka 50, miezi 11 na siku 13,” alisema Mgawe na kufafanua kuwa jenerali huyo alizaliwa mwaka 1925, Kijiji cha Nyamwaga, Tarafa Igwe Tarime, mkoani Mara.
Msemaji wa Jeshi la Wananchi Tanzania ( JWTZ), Kanali Kapambala Mgawe alithibitisha kutokea kwa kifo hicho akieleza kuwa Jenerali Mwita Kyaro alifariki dunia saa 4 asubuhi jana katika hospitali ya Bugando alipokuwa akitibiwa.
Akieleza wasifu wa marehemu huyo, Mgawe alisema Jenerali Kyaro aliongoza jeshi hilo akiwa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama (CDF) kati ya mwaka 1988 hadi 1994 alipostaafu.
“Jenerali Kyaro alistaafu akiwa amelitumikia jeshi kwa miaka 50, miezi 11 na siku 13,” alisema Mgawe na kufafanua kuwa jenerali huyo alizaliwa mwaka 1925, Kijiji cha Nyamwaga, Tarafa Igwe Tarime, mkoani Mara.
Tuesday, 10 April 2012
R.I.P KANUMBA...TUTAKUKUMBUKA DAIMA
Subscribe to:
Posts (Atom)







