Wednesday 1 January 2014

KWA MAISHA YA SASA KUFIKA MIAKA 50 NI NEEMA ZA MUNGU, NA MIAKA 50 YA NDOA NI HAKIKA UKUU WA MUNGU UNADHIHIRIKA KWA FAMILIA HII.

     Wakati binadamu wengi wakililia angalau kufika miaka Hamsini [50] angalau, katika umri wa kawaida. lankini pia fikiri binadamu mwenye umri wa miaka hamsini [50]  anaonekanaje hasa, wengi hujivunia hilo, lakini kwa familia hii ilijivunia tofati kabisa si umri wa kuishi kufikia hapa bali ni kufikisha miaka Hamsini ya Ndoa.
    Ndoa nyingi sana zimekua zikivunjika katika zama hizi na inapotokea unafikisha miaka kumi, ishirini, thelasini, arobaini  na hata Hamsini hakika ni kwa neema za Mungu tu.
   Hivi karibuni Familia ya Anthony Bahati ilishekherekea miaka Hamsini ya ndoa ndugu jamaa na marafiki walijumuika na familia hii kwa kumshukuru Mungu kwa kuilinda na kuisimamia familia hii iliyojaa upendo. wengi tunawaza kufika huko lakini yote ni kwa neema za Mungu.
  

TAZAMA PICHA WAKATI WA SHEREHE HIZO NYUMBANI KWA  FAMILIA YA ANTHONY BAHATI




No comments:

GEITA DOCUMENTARY

Contributors