Friday 15 February 2013

Goldie wa BBA afariki


Aliyekuwa mshiriki wa shindano la Big Brother Africa na mwanamuziki maarufu nchini Nigeria, Goldie Harvey amefariki ghafla jana kiwa hospitali baada ya kuugua kwa muda mfupi.

Goldie ambaye pia alikuwa na mahusiano ya kimapenzi na mwanamuziki nguli nchini Kenya, Prezzo amefariki akiwa anapatiwa matibabu katika hospitali ya Reddington, iliyoko katika visiwa vya Victoria, jijini Lagos, Nigeria.

Kwa mujibu wa gazeti la Daily Times, mwanamuziki huyo aliugua ghafla muda mfupi baada ya kutua Nigeria akitokea Marekani alipoenda kushuhudia tuzo za Grammy.

Taarifa za kifo chake pia zimethibitishwa na Lebo yake ya muziki ya Kennies Music kupitia mitandao ya kijamii ya Facebook na Twitter.

Goldie alikuwa mshiriki wa BBA mwaka 2012 ambapo alikutana na Prezzo na kuwa na mahusiano. Hivi karibuni katika kipindi cha televisheni cha ‘Churchill Live’, Prezzo alisema uhusiano wao ulikuwa katika hatua nzuri na alikuwa akijiandaa kulipa mahari.

1 comment:

Anonymous said...

Yesterday, while I was аt work, mу cousin stole my іPad
and tested to see іf it can survive а twenty five foot drop, just sо she can be a youtube sensation.
My apрle іpad is now ԁestroyed and she has 83
views. I know this is еntirely off topic but Ӏ had tο share it with someοne!
Review my web blog ... Viagra Without Prescription

GEITA DOCUMENTARY

Contributors