Thursday, 29 August 2013

PICHA: HARUSI YA MDOGO WETU FELISTER [LIKU] ILIYOFANYIKA MWISHONI MWA MWEZI HUU,

         Mwishoni mwa mwezi huu mdogo wetu Felister a.k.a LIKU alifunda pingu za maisha na Mume wake Daudi, harusi hiyo ilihudhuliwa na watu mbambali akiwemo mkuu wa mkoa wa Mwanza Evarist Ndikilo na pia Mh, Vicky Kamata ambae ni mbunge viti maalum Geita. na Baadhi ya Maofisa mbalimbali wa Serikali na wageni kutoka ndani na nje ya nchi.
          Harusi hiyo ilianza kwa Send off iliyofanyika kijijini kwa Bibi Harusi Geita na baadae kufuatiwa na Harusi iloyofana iliofanyikia Bunda mkoani mara nyumbani kwa Bwana harusi.

                               HIZI BAADHI YA PICHA KATIKA SEND OFF

Bibi Harusi Felister [Liku]


 Bibi Harusi Mtarajiwa akiingia ukumbini kwa ajili ya Send off.


Akijiandaa kukata keki na msindikizaji wake

Mh. Vicky Kamata Dada wa Bibi Harusi akiwa mwenye furaha alijumuika katika burudani ya muziki

Mjomba wa Bibi harusi ambaye pia ni Mkuu  wa Mkoa wa Mwanza Evarist Ndikilo akitoa nasaha kwa binti yake.

Wazazi wa Bibi harusi[ Mama wa Bibi harusi Helena Selemani wa kwanza kulia,, mjomba wa bibi harusi na mkuu wa mkoa wa Mwanza Evarist Ndikilo, Mama Mkubwa wa bibi harusi Paulina Selemani na Mama mdogo wa Bibi harusi Veronica Selemani.
Sehemu ya wahudhuriaji wakifuatilia kwa karibu

Bibi wa Bibi harusi akimpongeza mjukuu wake.

Mh. Vicky Kamata akitoa Nasaha kwa mdogo wake Liku.


kutoka kulia ni jaji mstaafu Anthon  Bahati, Mrs. Antony Bahati ambao ni babu na bibi wa Bibi Harusi, Mr&Mrs Evarist Ndikilo ,anaeyefuata ni Naibu mkurugenzi mkuu usalama wataifa bwana Zoka ambaye ni Baba wa Bwana harusi na Mkuu usalama taifa,mkoa wa Mwanza.na. kaka wa Bwana harusi,wa kwanza kushoto mstari wa mbele.


                           HIZI NI BAADHI YA PICHA  HARUSI HIYO HUKO BUNDA MARA

Bibi harusi akielekea kanisani

Wasindikizaji wakiwa tayari kumuongoza Bibi harusi kanisani
Bwana na Bibi Harusi wakisubiri mda wa kufunga ndoa

Hapa MUNGU ANAWAUNGANISHA NA KUWA MWILI MMOJA

Taratibu nyingine za harusi zikiendelea..
Mjomba wa Bibi harusi na Mkuu wa mkoa wa Mwanza Evarist Ndikilo na Dada yake ambaye ni Mama Mzazi wa Bibi Harusi Helena Selemani.
Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Evarist Ndikilo wakipongzana na naibu mkurugensi mkuu usalama wa taifa Bwana Zoka ambaye ni Baba wa Bwana Harusi na nyuma ni Mama wa bwana harusi Mrs Zoka.

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Evarist Ndikilo [mwenye Mic] ambae pia ni mjomba wa Bibi Harusi akitoa nasaha zake, Mama wa Bibi harusi Helena wa pili kutoka kushoto na mwisho ni Mr. and Mrs. Zoka ambao ni wazazi wa Bwana harusi.

Watoto wazuri wakiwa tayari kumsindikiza Bibi Harusi, wakiwa katika picha ya pamoja [kutoka kushoto] Glory Washington wa pili ni Anthoni Ndikilo wa tatu ni Irene Ndikilo, wa nne Jackline.

Anthoni Ndikilo na Glory Washington wakiwasindikiza Maharusi

Baadhi ya wahuduriaji akiwemo Vicky Kamata wakati wa kufunga ndoa kanisani



Kanisa ambapo ndoa hiyo ilifungwa
Hawa ni baadhi ya Ndugu wa Bibi Harusi, Wajomba, Mashemeji Na watoto wa Bibi harusi
kutoka kushoto ni Jacob kaka mkubwa wa bibi harusi, Mtoto wa Bibi Harusi Revocatus Washington, Erick Ndikilo Binamu wa Bibi harusi na Methew Masalu ambaye pia ni binamu wa Bibi harusi
kutoka kushoto ni Justa Dada wa Bibi harusi, Jacob Manyaga kaka wa Bibi harusi, Happyness Dada wa Bibi harusi na Teddy Dada wa Bibi harusi..

Monday, 26 August 2013

PICHA: HALI YA AMANI YAZIDI KUWA TETE NCHINI SYRIA,,"HALI INATISHA"

      Katik hali isiyo ya kawaida maelfu ya watu wanaendelea kupoteza maisha, huku wengine wakiambulia vilema vya maisha na wengine kuwa wakimbizi baada ya makazi yao kuharibiwa vibaya,, baadhi ya picha ilionyesha maiti nyingi zikiwa zimetapakaa mtaani.
       Lakini baya zaidi ni pale vijana wadogo sana wa makadrio kati ya miaka 12 hadi 17 wakiingia nao vitani na wengine wakionekana mitaani wakiw na silaha nzito kwa ajili ya mapambano..
   HII HALI NI TETE NA MBAYA SANA NA HILI NI SWALI LA KUJIULIZA SIASA ZA KWETU NAZO ZINAKWENDA WAPI?,

     HIZI NI BAADHI YA PICHA ZIKIONESHA HALI TETE  ILIYOPO NCHINI SYRIA KWASASA.

Watoto wadogo wakiwa Vitani
Umejenga nyumba kubwa kwa gharama na miaka mingi lakini dakika moja tu inakuwa sio nyumba tena ni kifusi..

Thamani ya nymba yoote lakini vita vimeileta hapa ilipo sasa
wanajeshi watoto wakishangilia mauaji kwao ni furaha akili na damu imebadilika na kua ya wanyama

hali ikiwa tete kila kona ya syria

watoto wakiwa na bunduki ya matoy zimekua kama manati tu kwao wakijianda kuingia vitani

Watoto wasiokuwa na hatia wanaendelea kuangamia kila kukicha kisa mtu mmoja amekataa kuondoka madarakani,, inauma sana

wanajeshi wakiendelea na uharibifu na mauaji hku wakifurahia wanachokifanya

Pata picha umentuma mwano dukani njiani anakutana na rocket ronger anafariki na hasa akiwa ni mwanao wa pekee, haya yamemkuta mtu huyu ambae hakufahamika mara moja

Mahali unapoishi panapokuwa kama Jehanam hapakaliki tena unakuwa mtumwa katika nchi yako mwenyewe
wanajeshi wakishangilia ushindi wa pili kulia akionekana bado ni kijana mdogo sana

Maiti kila kona ya mji mkuu wa syria kwa mbali nchi inaonekana kuwa saafi lakini hali ya mambo sasa imekua chungu na haikaliki tena

Kila mahali ni vita tu
Milipuko ya mabomu kila kukicha, na nchi inaendelea kuharibika vibaya..

Wednesday, 21 August 2013

RAIS JAKAYA KIKWETE AFANYA MABADILIKO YA MAKATIBU WAKUU NA MANAIBU WAKE..

RAIS J.M. KIKWETE
     RAIS Jakaya Kikwete amefanya mabadiliko ya uongozi katika ngazi za juu za utendaji wa Serikalini kwenye nafasi za Makatibu Wakuu na Naibu Makatibu Wakuu katika Wizara mbalimbali, ambapo  wapo waliohamishwa, wataopangiwa kazi nyingine na yumo anayestaafu.

Kauli hiyo ilitolewa leo jioni na Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue wakati akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam.

“Rais amefanya mbadiliko haya kwa lengo kuu la kuimarisha utendaji wa kazi za Serikali katika ngazi hizo za juu,” alisema Balozi Sefue.

Mabadiliko yaliyofanywa kwa upande wa Makatibu Wakuu ni kama ifuatavyo:

Katibu mkuu kiongozzi Balozi OMBENI SEFUE
  • Dk Florens Turuka amekuwa Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu, awali alikuwa Katibu Mkuu Wizara ya Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia.

  • Joyce Mapunjo amekuwa Katibu Mkuu Wizara ya Ushirikiano wa Afrika Mashariki, awali alikuwa Katibu Mkuu Wizara  ya Viwanda, Biashara na Masoko.

  • Jumanne Sagini amekuwa Katibu  Mkuu  Ofisi ya Waziri Mkuu - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) awali alikuwa Naibu Katibu  Ofisi wa Waziri Mkuu - TAMISEMI.

  • Dk Servacius Likwalile amekuwa Katibu Mkuu Wizara ya Fedha, awali alikuwa Naibu Katibu Wizara ya

Fedha.

  • Dk Patrick Makungu amekuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, awali alikuwa  Naibu Katibu Mkuu katika Wizara hiyo.

  • Alphayo Kitanda amekuwa Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, awali alikuwa Naibu Katibu Ofisi ya Waziri Mkuu – TAMISEMI.

  • Dk Shaaban Mwinjaka amekuwa Katibu Mkuu Wizara ya Uchukuzi, awali alikuwa Naibu Katibu Mkuu Wizara  ya Viwanda, Biashara na Masoko.

  • Dk Uledi Mussa amekuwa Katibu Mkuu Wizara  ya Viwanda, Biashara na Masoko, awali alikuwa Wizara ya Ushirikiano wa Afrika Mashariki. 

  • Profesa Sifuni Mchome amekuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya  Elimu na Mafunzo ya Ufundi, awali alikuwa Katibu Mtendaji Mkuu wa Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania.

  • Charles Pallangyo amekuwa Katibu Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, awali alikuwa Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri.

  • Anna Maembe amekuwa Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto, awali  alikuwa Naibu Katibu Mkuu wizara hiyo.

  • Sihaba Nkinga amekuwa Katibu  Mkuu wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, awali alikuwa Naibu Katibu Mkuu Wizara hiyo.

  • Sophia Kaduma amekuwa Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo, Chakula na Ushirika, awali alikuwa Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo.

Balozi Sefue aliongeza kwamba:

  • Katibu Mkuu aliyepewa uhamisho ni  Peniel  Lyimo ambaye anahamia Ofisi ya Rais - Ikulu  kwenye “Presidential’s Delivery Bureau” kama Naibu Mtendaji Mkuu mwenye jukumu la kuanzisha na kuongoza Idara ya Mageuzi ya Kilimo mwanzoni alikuwa  Katibu Mkuu  Ofisi ya Waziri Mkuu.

Makatibu wakuu watakaopangiwa kazi nyingine ni:-

  • Sethi Kamuhanda aliyekuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo 

Sunday, 18 August 2013

VIONGOZI SADC WAMPIGIA SALUTI RAIS KIKWETE, "JOYCE BANDA NAE ANENA"ATAKA WANWAKE WAPEWE NAFASI"

Baadhi ya wakuu wa SADC

           RAIS wa Malawi, Joyce Banda amempongeza Rais Jakaya Kikwete kwa kuimarisha demokrasia, amani na usalama katika nchi za Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za kusini mwa Afrika (SADC).
           Banda alitoa pongezi hizo wakati akihutubia Mkutano wa 33 wa Wakuu wa SADC baada ya kukabidhiwa nafasi ya uenyekiti wa jumuiya hiyo kutoka kwa Rais wa Msumbiji, Dk Armando Guebuza.
        “Wananchi wa Malawi, mimi na SADC tunampongeza Kikwete kwa kuimarisha amani, demokrasia na usalama katika jumuiya katika kipindi chake cha uongozi (wa Asasi ya Siasa,Ulinzi na usalama “Pia Rais wa Msumbiji, Armando Guebuza katika uongozi wake wa uenyekiti alishirikiana na Kikwete kushughulikia matatizo ya kisiasa na kuufanya ukanda wa nchi za SADC kuwa na amani,” alisema Rais Banda, ambaye nchi yake ina mgogoro na Tanzania upand wa ziwa Nyasa.
        
Rais Kikwete na Rais Joyce Banda wa Malawi
  Mgogoro huo uliibuka baada ya Serikali ya Malawi bila kushauriana na Tanzania, kutoa leseni kwa kampuni mbili za kigeni, kutafuta mafuta katika eneo la Ziwa upande wa Tanzania na kuibua mgogoro huo.
       Chanzo cha mgogoro huo unaoshughulikiwa na jopo la marais wastaafu wa Afrika; Thabo Mbeki (Afrika Kusini), Joachim Chisano (Msumbiji), Festus Mogae (Botswana) na wanasheria saba wa kimataifa, ni mikataba yenye utata iliyoachwa na wakoloni. Alisema ambao ndo waloigawa mipaka hiyo wakati wa ukoloni.
       Katika kipindi cha mwaka mmoja cha uongozi wa Rais Kikwete katika asasi hiyo ya siasa, ulinzi na usalama aliweza kufanikisha kufanyika kwa uchaguzi mkuu wa Zimbabwe, ambao Robert Mugabe ameshinda kuingoza nchi hiyo kwa muhula mwingine na kumbwaga mpinzani wake mkubwa na aliyekuwa waziri mkuu Morgan Tvshangirai.
      Amefanikisha pia kuanza kwa mchakato wa amani na kuatikana kwa muafaka wa kisiasa nchini Madagascar.
    Pia katika kipindi chake, alifanikisha kupelekwa kwa wanajeshi wa kulinda amani katika mji wa Goma, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) ambapo waasi wa M23 wanapambana na wanajeshi wa serikali. Wanajeshi hao wa kulinda amani wametoka Tanzania, Malawi na Afrika Kusini.

        Rais Kikwete amekabidhi madaraka hayo jana kwa Rais wa Namibia, Hifikepunye Pohamba. Rais huyo wa Malawi Bi. Joce  Banda ameahidi amani, Akizungumzia mkakati wake wakati wa uongozi wake wa mwaka mmoja kama Mwenyekiti wa SADC, Banda alisema ili ukanda wa SADC uwe na amani na usalama ni lazima nchi wanachama zipambane na umasikini.

       “Lazima tuimarishe siasa za ndani za nchi zetu, tuwe wavumilivu wa kisiasa na tusaidie wanawake wasiwe nyuma,” alisema. Aliahidi kuimarisha jumuiya za kikanda pamoja na kilimo kwa maelezo kuwa kilimo ndicho mwajiri mkuu wa wananchi wa nchi za SADC.
“Nitahamasisha kilimo kiboreshwe ili wananchi wa SADC waweze kuendesha kilimo cha biashara na pia sekta binafsi waingie kwenye kilimo na tupate masoko mapya ya bidhaa za kilimo nje ya mipaka ya ukanda wetu”.
      Alitaka katika ukanda wa jumuiya ya SADC kuboreshwe mwingiliano wa wananchi wa nchi za ukanda huo. Alisema haiwezekani kuboreshwa kwa jumuiya za kikanda bila kuruhusu mwingiliano huru wa wananchi wake.
     Rais Banda alitaka wanawake wapewe nafasi katika uongozi na kujengewa uwezo katika kuimarisha uchumi na kuondokana na umasikini na kusisitiza kuwa, “wanawake ndiyo wanaopambana na umasikini, wanabakwa, wanakabiliwa na unyanyasaji na wengi wamepoteza utu wao”.

      Kwa upande wa Mwenyekiti wa Kamisheni ya Umoja wa Afrika (AU), Dk Nkosazana Dlamini- Zuma alizitaka nchi za Afrika kuimarisha miundombinu ili mazao ya wakulima yaweze kusafirishwa pamoja na kuboreshwa kilimo, uwekezaji na kujengwa kwa viwanda.“Lazima tufanye kazi pamoja kuwahakikishia chakula watu wetu wa SADC na Afrika haiwezi kuendelea bila kuweka wanawake kila maeneo na kutafuta ufumbuzi wa changamoto zinazotukabili za tatizo la ajira kwa vijana, umasikini, sekta duni ya viwanda na tatizo la kutokuwepo usawa wa kijinsia,” alisema Zuma.



Wednesday, 14 August 2013

NECTA: MITIHANI KUSAHIHISHWA KWA COMPUTER, ITAONGEZA UBORA WA USAHIHISHWAJI.



Joyce Ndalichako

          Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani la Taifa (Necta), Dk Joyce Ndalichako amesema baraza lake linajiandaa kutumia teknolojia ya kompyuta wakati wa kusahihisha maswali ya mitihani ambayo wanafunzi wanajibu kwa kujieleza.
Kwa sasa teknolojia ya usahihishaji kwa kompyuta inayotumika nchini ni ile ya kujibu maswali ya kuchagua tu ya`Optical Mark Reader’ (OMR) iliyoanza kutumika mwaka jana kusahihisha mitihani ya darasa la saba.
     
Akizungumza na mwandishi wa habari jana wakati wa Mkutano wa Mabaraza ya Mitihani Afrika (AEAA), unaoendelea mjini hapa, Dk Ndalichako alisema: “Kwa kuanzia, Necta itafanya majaribio ya teknolojia hiyo mwakani na ninaamini itaongeza ubora katika usahihishaji.”
“Kwa kutumia hii teknolojia msahihishaji hawezi kuona namba ya mwanafunzi, anachoona ni sehemu ya swali anayotakiwa kusahihisha na jibu lake, akimaliza swali moja jingine linakuja moja kwa moja,” aliongeza.
   Alisema kwa kutumia teknolojia hiyo, mratibu wa usahihishaji anaweza kuona kazi inayofanywa na msahihishaji yeyote na hata kuwapima kama atakuwa na wasiwasi wowote.
    Alisema Zimbabwe imeanza kutumia teknolojia hiyo aliyosema itasaidia kuongeza ubora katika suala la usahihishaji.
     Akizungumza na waandishi wa habari wakati wa ufunguzi wa mkutano huo jana, alisema teknolojia ya OMR imeongeza ubora wa hali ya juu kwenye mtihani wa darasa la saba pamoja na usahihishaji wake.
“ Watu wanasema kuwa mtihani wa maswali ya kuchagua ni mrahisi, lakini hii siyo kweli, inatungwa na wataalamu na inalenga kumpima mtoto katika kila nyanja, ndiyo maana hata mtihani wa darasa la saba mwaka jana ilibidi Serikali ishushe alama za kwenda kidato cha kwanza zikawa 70 badala ya 100,” alisema Dk Ndalichako.
        Akizungumzia teknolojia hiyo, Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Philipo Mulugo alisema wamebaini kuwa zaidi ya asilimia 80 ya nchi za Afrika zinatumia mfumo wa usahihishaji kwa OMR.
    Alisema baadhi ya nchi zimeanza kusahihisha kwa kutumia kompyuta hata katika maswali ya kujieleza na kuwataka Watanzania kuacha kujirudisha nyuma.

Sunday, 11 August 2013

Mh. VICKY KAMATA NA VICTORIA FOUNDATION KWA UJUMLA WAWAPONGEZA WAISLAM DUNIANI KOTE

Mh. Vicky Kamata
 Familia ya Mh. Vicky Kamata
     Ikiwa ni siku moja baada ya sikukuu ya IDI el fitri Familia ya  Mh. Vicky Kamata ambaye pia ni mbunge wa viti maalum Geita pamoja na Mfuko wake wa VICTORIA FOUNDATION, wamewapongeza waislamu wote duniani kwa kusheherekea sikukuu ya IDI EL FITRI kwa amani na utulivu.  Akitoa pongezi hizo Mh. Vicky alisema "huu ni mfano wa kuigwa katika kila sikukuu ili kuweza kulinda amani ya taifa na Dunia kwa ujumla.."   
        Waislamu wote duniani siku ya Ijumaa na Jumamosi walisheherekea sikukuu hiyo baada ya kumaliza mfungo wa mwezi mtukufu wa Ramadhani.. sikukuu hiyo huadhimishwa na waislamu wote duniani kila mwaka na huendana na mwandamo wa mwezi...


GEITA DOCUMENTARY

Contributors