Friday, 2 April 2021

MAKALA MAALUM KWA WAFUGAJI WA KUKU: ZIFAHAMU TARATIBU NA RATIBA ZA UCHANJAJI WA KUKU KUANZIA VIFARANGA NA KUKU WAKUBWA.


Mtaalam wa Mifugo akiwapa chanjo vifaranga.
TARATIBU NA RATIBA ZA UCHANJAJI
    Wakati wa kutayarisha mpango wa kuchanja kuku kwa ajili ya kinga dhidi ya magonjwa, kuna vipengele vikuu sita Ambavyo unatakiwa uvifahamu na kuvizingatia. Vipengele hivyo ni kama ifuatavyo:
Kuku wakienyeji ni rahisi sana kuwafuga tofauti na wakisasa.
1. Vifaranga vinavyoanguliwa kwa pamoja:
 Iwapo una kundi zaidi ya moja la vifaranga wanaoanguliwa,
Weka utaratibu wa chanjo ambao utapunguza uwezekano wa magonjwa kuenea shambani. Hivyo basi,
Zipo namna nyingi za uchanjaji wa kuku zingine zinahitaji utaalam
Hakikisha vifaranga na kuku wote wanapata chanjo kwa pamoja.
2. Umri wa kuchanja kuku:
Kwa kuku ambao wanatarajiwa kutaga mayai au kuwa kuku wazazi, chanjo
nyingi hutolewa si zaidi ya mwezi mmoja kabla ya kuku kuanza kutaga. Pia kuna baadhi ya chanjo ambazo haziruhusiwi kwa kuku wadogo. (Angalia Ratiba).
3. Magonjwa muhimu katika eneo husika:
Ni muhimu sana kuelewa magonjwa ya kuku yaliyopo katika eneo lako kabla ya kuandaa programu ya uchanjaji, hasa kwa yale magonjwa ambayo chanjo zenye
Vimelea hai hutumika. Hivyo basi, sio busara kuanza kutumia chanjo za aina hii katika maeneo ambayo
Ugonjwa huo haujawahi kuripotiwa.
4. Hali ya kiafya ya kuku watakaochanjwa:
 Usiwape chanjo kuku ambao wanaonyesha dalili za kuathirika kwa mfumo wa hewa au wanaonyesha kuwa na minyoo au wadudu wengine. Kwa kuku walio na dalili hizi chanjo zinaweza kuleta madhara na zisifanye kazi.
5. Aina ya kuku watakaochanjwa:
Kuku wanaofugwa kwa ajili ya nyama wanahitaji kinga ya muda mfupi, hivyo basi chanjo moja inaweza kutosha kabla ya kufikia umri wa kuuzwa. Lakini kuku wa mayai na kuku wazazi wanahitaji programu ya chanjo ambayo itawakinga na magonjwa kwa kipindi chote wanapokua na kutaga. (Zingatia Ratiba).
6. Historia ya Magonjwa katika shamba:
Kabla ya kuandaa mpango wa chanjo, lazima ufahamu ni
Magonjwa gani yaliyoenea katika shamba.
a) Kama unataka kuingiza kuku wapya kutoka mahali ambako ugonjwa umeshawahi kutokea,
kuku hao wachanjwe wiki 3 kabla ya kuwaingiza shambani
b) Iwapo utatumia chanjo yenye vimelea hai, hakikisha kwamba magonjwa hayo yameshawahi
kutokea katika shamba husika. Usitumie chanjo hizi katika shamba ambalo ugonjwa huo
haujawahi kutokea au kutambuliwa.
c) Wasiliana na mashamba jirani kufahamu iwapo wanatumia chanjo zenye vimelea hai. Toa taarifa
kwa mamlaka za mifugo iwapo unapanga kutumia chanjo hizo katika eneo lako. Pata ushauri wa daktari.

TARATIBU ZA UCHANJAJI
Mambo muhimu ya kuzingatia:                                                                                         
  •Hakikisha unazingatia kwa makini masharti ya mtengenezaji wa chanjo: jinsi ya kuhifadhi, kutayarisha na njia inayotumika kumchanja kuku. Wakati wote zingatia masharti ya mtengenezaji kuhusu uhifadhi wa chanjo ili isipoteze nguvu.                                                     
                     

Thursday, 16 March 2017

VICTORIA FOUNDATION YATILIANA SAINI NA YAMOTO BAND KATIKA KUFANIKISHA PROGRAM YA "FOR THEM"

Na Steven Mruma


       Leo mkurugenzi na mwenyekiti wa Victoria Foundation ametiliana saini mkataba wa pamoja wa kuanikisha program maalum ya  "FOR THEM" na kundi la muziki wa kizazi kipya la Yamoto Band. Mkataba huo utawezesha kuhamasisha na kufanikisha program maalum kwa ajili ya watoto yatima wajane pamoja na waemavu. Mkataba huo umetiwa saini Jijini Dar es salam katika ofisi zaVictoria Foundation kati ya mwenyekiti wa Victoria Foundation na mbunge wa viti maalum mkoa wa Geita Mh. Vicky Kamata Likwelile na Kiongozi wa Yamoto Band.





Saturday, 11 March 2017

VICTORIA FOUNDATION YAGAWA MASHUKA 100 HOSPITAL YA MKOA WA GEITA


Tarehe 10.03.2017
Mhe Vicky Kamata Likwelile Mbunge wa viti maalum Mkoa wa Geita amefanya ziara na kugawa mashuka 100 katika hospitali ya Mkoa wa Geita kwenye ward ya akina mama na watoto,
Aidha Mhe Vicky Kamata Likwelile amesikiliza changamoto mbalimbali za wagonjwa ikiwemo tatizo la upungufu wa vitanda pamoja na ward za akinamama.
Lakini pia amesikiliza changamoto mbalimbali toka kwa watumishi wa hospital hiyo ikiwemo suala la uchache wa wahudumu wa afya na Madaktari ikiwemo madaktari wa magonjwa ya akina mama na watoto.
Mhe Vicky Kamata Likwelile ameahidi kuzifanyia kazi changamoto hizo.
Katika ziara hiyo ya Mhe Vicky Kamata Likwelile aliambatana na viongozi wa wa UWT akiwemo Mhe Maimuna Mingisi (DV) Mwenyekiti wa UWT Mkoa wa Geita na Ndugu Mazoea Salum Katibu wa UWT Wilaya ya Geita.
Mhe Vicky Kamata amewashukuru madaktari na wauguzi wa Hospitali hiyo na kuwapongeza kwa kazi nzuri wanazofanya za kuwahudumia wagonjwa.
Imetolewa na
Mazoea Salum
Katibu wa UWT
Wilaya ya Geita
Imehaririwa na Steven Mruma Jr.






Friday, 10 March 2017

MH. VICKY KAMATA APOKEA TUZO YA HESHIMA KWA KUPIGANIA HAKI ZA WANAWAKE

Na Steven Mruma 

   Mh. Vicky Kamata Likwelile amepokea tuzo ya heshima kwa kutambulika kwa mchango wake mkubwa alio uonyesha kwa jamii ya wanawake wa Tanzania na kanda ya ziwa kwa kupitia nafasi zake aizonazo kama Mbunge, lakini pia kama mwanamuziki hasa kupitia wimbo wake wa "Wanawake na Maendeleo" na pia kupitia tasisi yake ya Victoria Foundation. 
   Tuzo hizo zimetolewa na NITETEE WOMAN AWARD hafla iliyofanyika jijini mwanza na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wanawake akiwemo naibu waziri wa nyumba na maendeleo ya makazi Angeina Mabula









Saturday, 16 January 2016

HIGHER EDUCATION EXHIBITION


THE TANZANIA COMMISSION FOR UNIVERSITIES

8th Exhibitions on Higher Education, Science and Technology

Diamond Jubilee Hall, Dar es Salaam

Wednesday 22th to Friday 24th May, 2013

The Tanzania Commission for Universities (TCU) wishes to inform all stakeholders and the general public that, the 8th exhibitions on Higher Education, Science and Technology will be held from 22nd-24th May 2013. These exhibitions are jointly organized by the TCU, the Ministry of Education and Vocational Training (MoEVT), Higher Education Institutions, as well as Regulatory, Professional and Research Bodies in and outside Tanzania.


Theme: "Building a knowledgeable, accountable and progressive society through Higher Education, Science and Technology"


Exhibitions’ Vision:

To become the leading national and regional state of the art exhibitions that promotes participation, enhances collaboration, builds up partnerships between higher education institutions and the Industry as well as developing mutual understanding on the issues that govern the quality of Higher education in the Country for the benefit of all humanity.

GEITA DOCUMENTARY

Contributors