Tuesday, 21 May 2013

MSAFARA WA FISTULA INATIBIKA WAELEKEA GEITA



Katika kuelekea kuadhimisha siku ya Fistula Duniani, 23/5/2013, Vodacom kwa kushirikiana na taasisi ys CCBRT wameandaa safari ya kuzunguka nchi nzima inayofahamika kama ‘Fistula Inatibika’ kutokea Bukoba hadi Dar es Salaam kwenye kilele cha maadhimisho ya siku hiyo kwenye viwanja vya CCBRT yatakayopokelewa na Rais Jakaya Kikwete.

Safari hiyo ambayo inahusisha pia kupita kwenye sehemu mbalimbali kuwapa wananchi ujumbe kuwa Fistula inatibika, itajumuisha pia kukusanya ujumbe kutoka kwa familia zilizoathirika na Fistula kupeleka kwa Rais hapo tarehe 23 ya mwezi huu.
Msafara huo utakaochukua jumla ya siku saba, unaongozwa na mwanamuziki wa kizazi kipya, Hamis Mwinjuma maarufu kama Mwana FA, ambaye atakuwa akiwapa elimu kuhusiana na Fistula wananchi wa sehemu tofauti tofauti watakaopitiwa na msafara huo.

Meneja Uhusiano wa Mambo ya Nje wa Vodacom Bwana Salim Mwalimu akimkaribisha Mkuu wa Mkoa wa Kagera kwenye kampeni ya Fistula Inatibika

MwanaFA akiwaelimisha wananchi wa Geita na kuwahamasisha kutumia fursa hii kujitokeza ili waweze kutibiwa bure

Familia yenye furaha iliyofanikiwa kuushinda ugonjwa wa Fistula kutokana na juhudi za hospitali ya CCBRT pamoja na Vodacom Foundation

Wakazi wa Geita waliojitokeza kwenye kampeni ya Fistula Inatibika

Habari na bongolookup blog

STRUGGLE FOR MANDELA'S WEALTH


 The daughter's of South Africa's anti-apartheid icon & its founding President Nelson Mandela have sued their father over rights to his huge collection of artwork & millions of rands.

 Zenani and Makaziwe Mandela intend their father's 2004 decision to bar the duo's lawyer to stop managing his financial, personal and legal affairs. Mandela, the ailing 92yr old freedom fighter is adored world over $ is said to be worth at least a billion rands in franchise.

A few months ago, the two sisters sued George Bizos, one of Mandela's close & longtime friend to have him kicked out of the Mandela Trust.

Sunday, 21 April 2013

MH. VICKY KAMATA AZINDUA 'VICKY KAMATA CUP' MKOANI GEITA

Mbunge wa Viti Maalum (CCM)mkoa wa Geita Mh. Vicky Kamata leo amezindua rasmi mashindano ya Vicky Kamata Cup mkoani humo. Mashindano hayo yanazikutanisha timu kutoka kata zote za mkoa wa Geita.
 Jezi zilizotolewa na Mh Vicky Kamata kwa timu zote zinazoshiriki ligi hiyo.


     Timu zikiwa zinajiandaa kwa ajili ya kuanza kwa mchezo

Friday, 19 April 2013

WAGENI NA WAFADHILI WA VICTORIA FOUNDATION WALIPOMTEMBELEA MH. WAZIRI MKUU DODOMA



 Kutoka kushoto ni mfanyabiashara mkubwa kuotoka U.A.E-Dubai Mr. Niaz Wal Khan,Mwenyekiti wa Victoria Foundation Ms. Vicky Kamata,Mkurugenzi mtendaji wa Sayed Corporation Tz Mr.Sayed Masood,Waziri mkuu Mh. Mizengo Pinda,Mfanyabiashara toka Dubai Mr. Haji Badshah Wazir,Mr. Salami na Manager wa Sayed Corporation tawi la Uganda Mr. Abdallah wakiwa katika picha ya pamoja.

 Mr.Haji Badshah Wazir akijadiliana jambo na Waziri mkuu Mh. Mizengo Pinda walipomtembelea huko Dodoma.
Mwenyekiti wa Victoria Foundation Mh. Vicky Kamata (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na wafadhili wa Victoria Foundation toka U.A.E-Dubai Mr. Haji Badshah Wazir na Mr. Niaz Wal Khan (Kushoto)

GEITA DOCUMENTARY

Contributors