Monday, 19 November 2012

HUAWEI YAZINDUA MPANGO WA TEKNOHAMA KATIKA SEKTA YA ELIMU NCHINI



 
Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia Profesa Makame Mbarawa akizungumza na wageni waalikwa wakati wa uzinduzi wa mpango kabambe wa Teknohama katika Sekta ya Elimu nchini uliofadhiliwa na Kampuni ya HUAWEI kutoka China leo.
Katika Mradi huo wa Teknohama itayowezesha Watanzania mbalimbali kutoka shule za Sekondari na Vyuoni kupata vifaa na mafunzo ya Sayansi na Teknolojia ili kusukuma mbele maendeleo katika nyanja za Uchumi na Kijamii.
 
Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya HUAWEI kutoka China Bw. Bruce Zhang akizungumza katika hafla hiyo kwamba Mpango huu unaoitwa "Huawei ICT Star" itasaidia katika shule za Primary na Sekondari katika kusukuma mbele maendeleo ya Sayansi na Teknolojia nchini Tanzania.
Alisema katika Program hii itasaidia kuboresha miundo mbinu katika Sanyansi na Teknolojia ili kutoa mwamko kwa vijana wa Kitanzania kujifunza masomo ya Sayansi na Teknolojia. 
Balozi wa China nchini Tanzania Mh. LU YOUQING akitoa maelezo yake wakati wa uzinduzi wa mpango wa Teknohama katika shule na vyuo nchini Tanzania.
Balozi alisema mpango huu ni mwendelezo wa uhusiano mwema kati ya Tanzania na Jamhuri ya watu wa China katika nyanja mbalimbali za biashara uchumi na Kijamii.
Aliongeza kwamba Serikali ya China itaendelea na mikakati yake ya kusaidia nchi ya Tanzania ili kuweza kufikia malengo ya Milenia ya 2015. 
Mgeni rasmi Mh. Mbarawa na Balozi wa China wakizindua rasmi mpango wa "HUAWEI ICT STAR" nchini Tanzania. 
Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia Profesa Mbarawa na Mkurugenzi Mtendaji wa HUAWEI Bw. Bruce Zhang wakitiliana saini kitabu cha makubaliano rasmi ya Ushirikiano katika Sekta ya Sayansi na Teknolojia kupitia Elimu.
 
Meza Kuu.
 
Pichani Juu na Chini ni wageni waalikwa waliohudhuria uzinduzi huo.
 
Profesa Mbarawa akikabidhi zawadi kwa Mkurugenzi Mtendaji wa HUAWEI. 
 
Mgeni rasmi Waziri Mbarawa akiondoka ukumbi baada ya uzinduzi.
 
 Kwa hisani ya johnbadi.blogspot.com 

Friday, 16 November 2012

HEALTH BENEFITS OF DRINKING CAMEL MILK



Camel milk, used medicinally for centuries by nomadic people, is the closest to human mother's milk and contains 10 times more iron and three times more vitamin C than cow's milk, according to The Huffington Post. Camels possess unique, powerful immune-system components, which are contained in their milk. Camel milk might potentially benefit disorders including diabetes and autism. As with any natural remedy, consult your doctor before drinking camel milk.

Thursday, 15 November 2012

MIZENGO PINDA KUONGOZA SEMINA KWA MA-RC, DC



WAZIRI Mkuu, Mizengo Pinda, leo anarajiwa kuongoza warsha ya uhamasishaji kuhusu majadiliano ya ushirikiano kwa manufaa ya wote (Smart Partnership Dialogue) kwa wakuu wote wa mikoa (ma-RC), makatibu tawala na wakuu wa wilaya (ma-DC) zote nchini.

Wednesday, 14 November 2012

KIKWETE MWENYEKITI TENA CCM, MANGULA, DK, SHEIN MAKAMU WAKE

Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete akipongezwa na aliyekuwa Msimamizi wa Uchaguzi wa Mwenyekiti wa CCM Taifa na Makamu wenyeviti wawili, Spika wa Bunge Anna Makinda, baada ya kumtangaza kushinda nafasi hiyo ya Uenyekiti, katika uchaguzi uliofanyika jana katika ukumbi wa Kizota, Dodoma, ikiwa ni kuhitimisha shughuli za Mkutano Mkuu wa Nane wa CCM. Wapili Kulia ni Makamu Mwenyekiti Mpya wa CCM (Zanzibar) Dk. Ali Mohamed Shein na Makamu wa Rais Dk. Mohamed Gharib Bilal
 Mwenyekiti wa CCM, Taifa, Jakaya Kikwete na Makamu wake wawili Rais wa Zanzibar, Dk. Ali Mohamed Shein (Zanzibar) na Philip Mangula (Bara) wakiwa meza kuu baada ya kutangazwa kushika nyandhifa zao.
 Wajumbe wakiserebuka baada ya Rais Jakaya Kikwete kutangazwa kuwa mshindi wa Uenyekiti wa CCM, Taifa.
 Mwenyekiti wa CCM, Jakaya Kikwete akiongoza kikao baada ya kushinda tena kiti hicho. Kushoto ni Makamu Mwenyekiti wa CCM (Zanzibar), Dk. Ali Mohamed Sheni na Makamu Mwenyekiti wa CCM Bara, Phili Mangula. 

                            PICHA ZOTE NA BASHIR NKOROMO
                                   www.ccmchama.blogspot.com 

MTANGAZAJI WA SIBUKA TV LULU OSCAR AMEFARIKI DUNIA

Marehemu LuLu Oscar enzi za uhai wake
              Mwenyezi Mungu ailaze roho ya Marehemu Lulu Oscar mahali pema peponi...

GEITA DOCUMENTARY

Contributors