Wednesday, 12 September 2012

WANAFUNZI CHUO CHA UANDISHI WA HABARI D'SALAAM (DSJ) WALIPOUNGANA NA WAANDISHI NCHINI KATIKA MAANDAMANO YA KULAANI MAUAJI YA MWANDISHI DAUD MWANGOSI

Wanafunzi wa Dar es Salaam School of Journalism wakiwa wamebeba ujumbe wao kulaani mauaji ya Daudi Mwangosi.Maandamano hayo yalifanyika jana mjini Dar es Salaam na katika baadhi ya mikoa nchini kote.

Tuesday, 11 September 2012

WAZIRI MKUU AZINDUA MRADI WA MATREKTA KWA WAJASIRIAMALI MKOANI GEITA

 Waziri mkuu Mizengo Pinda akizindua mradi wa matrekta kwa wajasiriamali wa kata ya Katoro jimbo la Busanda katika mkoa mpya wa Geita


ZIARA YA WAZIRI MKUU MKOANI GEITA

 Waziri mkuu Mhe. Mizengo Pinda akizindua Zahanati katika kata ya Senga mkoani Geita.Hafla hiyo ilifanyika jana ambapo waziri mkuu yupo mkoani humo kwa ziara ya kikazi
                     Pia hapakukosa kuwa na burudani ya Ngoma kwa Mhe. waziri mkuu      

Monday, 10 September 2012

Nyakua Nyakitita: Mhadhiri DIT anayeokota makopo barabarani


WASWAHILI siku zote husema hujafa hujaumbika! Ukweli wa usemi huu unatimia unapomwona mtu huyu.
Ungemwona miaka 13 iliyopita ungeshangaa, lakini leo mtu aliyeitwa mstaarabu, bondia wa kutegemewa na mcheza twist wa ukweli, Nyakua Nyakitita amebadilika kweli.

Mtu ambaye alikuwa mhadhiri wa kutegemewa katika Taasisi ya Teknolojia Dar es Salaam (DIT), msomi aliyebobea katika uhandisi, kazi aliyoianza katika miaka ya 1990, sasa anaishi kwa kuombaomba, kuchora ramani na mambo yasiyojulikana!

Leo hii, msomi huyo yuko katika hali ya kusikitisha ya uchafu uliokithiri, anashinda karibu na maeneo ya chuo hicho makutano ya Barabara za Morogoro na Bibi Titi Mohammed  huku akiokota makopo na takataka nyingine na mara nyingine akikusanya mawe na kuyapanga kwa kutengeneza michoro ya vitu mbalimbali ikiwamo ramani ya Tanzania na  kuandika majina ya marafiki zake.

Nini kilichomsibu hadi kufikia hapo? 
Kabla ya kupata matatizo ya akili mwalimu  na mhandisi Nyakua aliishi maisha mazuri tu ambayo kwa vijana wa sasa wanasema, ‘yalimtoa’ kwani alitembelea nchi kadhaa kwa ajili ya ziara za mafunzo au kozi ndefu na ambazo zilimpa fursa nzuri ya ‘kujirusha’.

Wednesday, 5 September 2012

MAREHEMU DAUD MWANGOSI AZIKWA KIJIJINI KWAO BUSOKA

Mjane wa marehemu Daud Mwangosi akilia kwa uchungu  juu ya kaburi la mumewe  mara baada ya  mazishi
 MAZISHI ya Mwandishi wa Habari, Daud Mwangosi yalifanyika jana katika Kijiji cha Busoka kilichoko wilayani Rungwe, Mbeya na kuhudhuriwa na mamia ya waombolezaji wakiongozwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Kazi Maalumu), Profesa Mark Mwandosya na Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Willibrod Slaa. 

Katika mazishi hayo, viongozi hao wawili kila mmoja alitangaza kuwasomesha watoto wa marehemu Mwangosi ambaye alifariki dunia Septemba 2, mwaka huu baada ya kupigwa na kitu kinachodhaniwa kuwa ni bomu wakati polisi walipokuwa wakisambaratisha mkutano wa Chadema.

Tuesday, 4 September 2012

KATIBA MPYA KUPATIKANA APRIL, 2014


TUME ya Mabadiliko ya Katiba imesema imejipanga kukamilisha majukumu yake ndani ya muda uliowekwa na Sheria ya Mabadiliko ya Katiba, hivyo nchi kuwa na Katiba Mpya ifikapo Aprili, mwaka 2014.

Mwenyekiti wa tume hiyo, Jaji mstaafu Joseph Warioba, aliwaeleza mawaziri wa Katiba na Sheria kutoka Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kuwa pamoja na changamoto zilizopo, dhamira hiyo ya tume ipo palepale.

Mawaziri hao, Mathias Chikawe wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Abubakar Khamis Bakari wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar walitembelea ofisi za Tume ya Mabadiliko ya Katiba jana, ili kujionea utekelezaji wa shughuli mbalimbali za tume hiyo.

GEITA DOCUMENTARY

Contributors