Friday, 20 April 2012

Kero ya umeme Dar kwisha...


SHIRIKA la Ugavi wa Umeme Nchini (TANESCO) limesema hakuna tatizo la nishati hiyo kwa wakazi wa Dar es Salaam na viunga vyake, baada ya kutengemaa kwa kituo kidogo cha usambazaji (substation) cha Upanga.
Akizungumza na Tanzania Daima jana, Meneja Mawasiliano wa Tanesco, Badra Masoud, alisema umeme hukatika mara kwa mara hususan maeneo ya Kimara ambako wakazi wake wanalilalamikia shirika hilo.
Aliwataka wakazi wa jijini hapa kuamini kwamba hakuna tatizo la umeme huku akibainisha kuwa kituo cha usambazaji kilichokua kikifanyiwa marekebisho cha Upanga kimetengemaa.
“Baadhi ya maeneo hasa Upanga na katikati ya jiji palikuwa na tatizo la umeme kwa sababu ya hitilafu kidogo kwenye ‘substation’ ya Upanga lakini sasa imerekebishwa hakuna tena tatizo. Mitambo yote inayozalisha umeme na iko kwenye hali nzuri ila kwenye hizo substation ambazo zinapokea na kusambaza umeme wakati mwingine zinaleta taabu lakini kwa sasa hakuna tatuzo,” alisema Badra.

Makamu wa Rais aipa somo mifuko ya jamii

MAKAMU wa Rais, Dk. Mohamed Gharib Bilal ameitaka mifuko ya hifadhi ya jamii kutoa kinga dhidi ya majanga ili kuhakikisha kuwa wanachama wake wanaishi vyema hata majanga yanapotokea. 

Dk. Bilal aliyasema hayo jana wakati akifungua Mkutano Mkuu wa Nne wa Wadau wa Mfuko wa Akiba wa Wafanyakazi wa Serikali (GEPF) uliofanyika jijini hapa. 

Thursday, 19 April 2012


MAOMBI YA KUPANDA KWA NAULI ZA DALADALA YATINGA SUMATRA


CHAMA cha Wamiliki wa Daladala MKoa wa Dar es SAlaam (DACOBOA)wamepeleka maombi yao Mamlaka ya Udhibiti Majini na Nchi Kavu (SUMATRA) kwa ajili ya kuongeza bei mpya ya nauli za daladala.
Maombi hayo ya kuongeza bei ya nauli mpya yametokana na madai ya wamiliki wa daladala Dar es Salaam kwamba  gharama za uendeshaji zimepanda.

GEITA DOCUMENTARY

Contributors