Friday, 13 April 2012

BABA MZAZI WA LULU ATAKA JAMII ISIMHUKUMU MWANAWE


BABA mzazi wa msanii wa filamu, Elizabeth Michael 'Lulu,' ameitaka jamii kutomhukumu mwanawe kutokana na kifo cha msanii mwenzake marehemu Steven Kanumba, badala yake iache vyombo vya sheria vifanye kazi yake.

Mzazi huyo, Michael Edward Kimemeta anayeishi mjini Moshi, amewaomba Watanzania kuiachia Mahakama iamue kama mtoto wao anahusika katika kifo hicho ama la.

Kimemeta, ameeleza kuwa binti yake ana umri wa miaka 16 tofauti na inavyoelezwa kuwa ana miaka 18.

MAONYESHO YA SABA YA VYUO VIKUU KUANZA APRIL 18


Maonyesho ya saba ya vyuo vikuu yatafanyika kuanzia tarehe 18 hadi 20 mwezi Aprili mwaka 2012 katika ukumbi wa Diamond Jubilee Upanga Dar es Salaam.
Mgeni rasmi atakuwa Makamu wa rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Dr. Gharib Bilali.
Maonesho yatakuwa yanafunguliwa saa tatu kamili asubuhi na kufungwa saa kumi na mbili jioni kila siku.
       'HAKUNA KIINGILIO NA WOTE MNAKARIBISHWA'

Thursday, 12 April 2012

Wizi wa kazi za wasanii waibua mjadala Bungeni


SUALA la wizi wa kazi za wasanii nchini, limeibua mjadala mkali bungeni huku Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Kabwe Zitto akipendekeza mtu atakayekamatwa akiuza CD na DvD feki za kazi za wasanii atozwe faini isiyopungua sh50 milioni.

Mbunge huyo ambaye pia ni Naibu Msemaji wa Kambi rasmi ya upinzani Bungeni, alipendekeza kuwa mtu yeyote atakayekutwa na kazi feki za wasanii naye aadhibiwe vikali ili kujenga Utamaduni wa Watanzania kuacha kununua kazi za wizi wasaniii.

Wabunge hao walichachamaa Bungeni mjini Dodoma jana wakati wakichangia hotuba ya Waziri wa Viwanda na Biashara, Dk. Cyril Chami kuhusu muswada wa sheria ya marekebisho ya sheria mbalimbali za biashara wa mwaka 2011.

Mutharika kuzikwa April 23


IKULU ya Malawi imethibitisha jana kuwa mazishi ya Rais wake wa tatu, Bingu wa Mutharika yatafanyika Aprili 23, mwaka huu katika shamba lake lililopo Ndata, Wilaya ya Thyolo, kusini mwa Mji wa Blantyre.

Uamuzi huo unakwenda sambamba na ule wa kuongezwa kwa siku za maombolezo kutoka 10 hadi 30, ili kuyapa maombolezo hayo uzito unaolingana na msiba wa “mkuu wa nchi aliyefariki dunia akiwa madarakani.”


Awali, kabla ya Rais Banda kuapishwa, Ofisi ya Rais na Baraza la Mawaziri (OPC) ya Malawi, ilitoa taarifa kwamba kungekuwa na siku 10 tu za maombolezo ambazo zilitarajiwa kumalizika Jumapili wiki hii.

Lakini kutokana na kuongezeka kwa siku 20 zaidi, maombolezo hayo yanatarajiwa kukoma ifikapo Mei 6, mwaka huu na katika kipindi chote hicho, bendera zitaendelea kupepea nusu mlingoti huku televisheni na redio zikipiga muziki wa maombolezo.

GEITA DOCUMENTARY

Contributors