WALIMU wanne wa Shule ya Msingi Hamkoko na msimamizi mmoja wa mitihani, wamefikishwa katika Mahakama ya Wilaya ya Ukerewe mkoani Mwanza kwa tuhuma za wizi wa mtihani wa taifa wa darasa la saba, huku Jeshi la Polisi likiendelea kumtafuta mwalimu mwingine aliyetoroka.